Swali: Kuna mwanamke aliacha kufunga Ramadhaan kwa muda wa miaka kumi kwa sababu ya mimba na kunyonyesha kwa sababu ya kuchelea afya na mtoto wake. Baada ya hapo akatubia. Je, tawbah inatosha au kuna kitu kingine kinachomlazimu?
Jibu: Ndio. Tawbah inatosha kwa sharti alipe yale masiku anayodaiwa. Akilipa masiku anayodaiwa itatosha. Halazimiki kulisha kwa mujibu wa maoni yaliyo na nguvu miongoni mwa maoni mbalimbali ya wanachuoni. Wako wanachuoni wanaosema mtu akila na akachelewesha kulipa mpaka akaingiliwa na Ramadhaan ya pili bila udhuru wowote basi ni wajibu kwake kulipa na kulisha. Lakini maoni sahihi ni kwamba halazimiki kulisha na kwamba kufunga kunamtosha.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (44) http://binothaimeen.net/content/1017
- Imechapishwa: 20/02/2019
Swali: Kuna mwanamke aliacha kufunga Ramadhaan kwa muda wa miaka kumi kwa sababu ya mimba na kunyonyesha kwa sababu ya kuchelea afya na mtoto wake. Baada ya hapo akatubia. Je, tawbah inatosha au kuna kitu kingine kinachomlazimu?
Jibu: Ndio. Tawbah inatosha kwa sharti alipe yale masiku anayodaiwa. Akilipa masiku anayodaiwa itatosha. Halazimiki kulisha kwa mujibu wa maoni yaliyo na nguvu miongoni mwa maoni mbalimbali ya wanachuoni. Wako wanachuoni wanaosema mtu akila na akachelewesha kulipa mpaka akaingiliwa na Ramadhaan ya pili bila udhuru wowote basi ni wajibu kwake kulipa na kulisha. Lakini maoni sahihi ni kwamba halazimiki kulisha na kwamba kufunga kunamtosha.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (44) http://binothaimeen.net/content/1017
Imechapishwa: 20/02/2019
https://firqatunnajia.com/ameacha-kufunga-miaka-10-kwa-sababu-ya-mimba-na-kunyonyesha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)