al-Khaliyliy amesema:
“Kuhusu dalili za kinakili – za wanaopinga kuonekana kwa Allaah – baadhi zinapatikana katika Qur-aan na zingine katika Sunnah.”[1]
Kisha akasema:
“Katika Qur-aan ni maneno Yake (Ta´ala):
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[2]
Halafu akasema:
“Dalili hapa ni kwamba (Ta´ala) amejisifu kuwa macho hayamdiriki. Kudiriki maana yake ni kuona. Ikapata kubainika kuwa kutoonekana kwa macho ni sifa ya kidhati yenye kulazimiana Naye (Ta´ala). Lau kungelikuwa kipindi anaonekana basi kujisifu Kwake kungeondoka na mambo yakishakuwa hivo inageuka kuwa kinyume chake ambacho ni kulaumika – Allaah ametakasika na hilo.”
Akaendelea kusema:
“Kwa upande mwingine ni kwamba [hapa] Allaah anaelezea sifa miongoni mwa sifa Zake na maelezo ya Allaah hayabadiliki. Lau ingelibadilika basi kubadilika kwake ingelikuwa ni kumkadhibisha:
وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللَّـهِ قِيلًا
“Na nani aliye mkweli zaidi kwa kauli kuliko Allaah?”[3]
Tunasema ni kweli kwamba ni maelezo ambayo hayakubadilika. Allaah amesema kuwa anaonekana lakini hata hivyo katika kuonekana huko hazungukwi (Subhaanahu wa Ta´ala) kutokana na ukubwa Wake. Hivyo ndivyo alivyosema Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa). Sivyo kama anavyoonelea al-Khaliyliy.
[1] Uk. 68
[2] 06:103
[3] 04:122
- Mhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ar-Radd al-Qawiym, uk. 102
- Imechapishwa: 14/01/2017
al-Khaliyliy amesema:
“Kuhusu dalili za kinakili – za wanaopinga kuonekana kwa Allaah – baadhi zinapatikana katika Qur-aan na zingine katika Sunnah.”[1]
Kisha akasema:
“Katika Qur-aan ni maneno Yake (Ta´ala):
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[2]
Halafu akasema:
“Dalili hapa ni kwamba (Ta´ala) amejisifu kuwa macho hayamdiriki. Kudiriki maana yake ni kuona. Ikapata kubainika kuwa kutoonekana kwa macho ni sifa ya kidhati yenye kulazimiana Naye (Ta´ala). Lau kungelikuwa kipindi anaonekana basi kujisifu Kwake kungeondoka na mambo yakishakuwa hivo inageuka kuwa kinyume chake ambacho ni kulaumika – Allaah ametakasika na hilo.”
Akaendelea kusema:
“Kwa upande mwingine ni kwamba [hapa] Allaah anaelezea sifa miongoni mwa sifa Zake na maelezo ya Allaah hayabadiliki. Lau ingelibadilika basi kubadilika kwake ingelikuwa ni kumkadhibisha:
وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللَّـهِ قِيلًا
“Na nani aliye mkweli zaidi kwa kauli kuliko Allaah?”[3]
Tunasema ni kweli kwamba ni maelezo ambayo hayakubadilika. Allaah amesema kuwa anaonekana lakini hata hivyo katika kuonekana huko hazungukwi (Subhaanahu wa Ta´ala) kutokana na ukubwa Wake. Hivyo ndivyo alivyosema Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa). Sivyo kama anavyoonelea al-Khaliyliy.
[1] Uk. 68
[2] 06:103
[3] 04:122
Mhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ar-Radd al-Qawiym, uk. 102
Imechapishwa: 14/01/2017
https://firqatunnajia.com/allaah-ataonekana-lakini-hatozungukwa-yeye-wote/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)