Swali: Kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Allaah Amemuumba Aadam kwa Sura Yake.”
Je, makusudio ni Sura ya Allaah?
Jibu: Bila ya shaka. Kuna Riwaayah nyingine:
“Allaah Amemuumba Aadam kwa Sura ya Ar-Rahmaan.”
Imekuja namna hii katika Riwaayah sahihi. Allaah (Jalla wa ´Alaa) Ana Sura, kama ilivyokuja katika Hadiyth:
“Nimemuona Mola Wangu katika Sura nzuri.”
Allaah Ana Sura.
Swali: Je, inajuzu kuiwekea taawili Sura sehemu hii?
Jibu: Hapana. Hadiyth inabaki katika maana yake na matamshi yake. Haibadilishwi.
Shaykh Hamuud at-Tuwayjiriy (Rahimahu Allaah) ameandika kijitabu kizuri kuhusu mada hii. Humo amewaraddi wale wanaitilia taawili Hadiyth hii. Kadhalika kuna maneno ya Shaykh-ul-Islaam kuhusiana na hili.
Swali: Je, imesihi kutoka kwa Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ya kwamba amesema “Kila mwenye kuwekea taawili Hadiyth hii ya Sura, basi huyo ni Jahmiy”?
Jibu: Kwa kweli mimi sijaona maneno ya Imaam Ahmad. Lakini maana yake ni sahihi. Ni kweli kwamba ni Jahmiyah. Hakuna anayepinga Sifa za Allaah (´Azza wa Jalla) isipokuwa Jahmiyyah. Miongoni mwa Sifa Zake ni Sura.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (42) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo--1432-03-10.MP3
- Imechapishwa: 16/11/2014