Swali: Vipi kumraddi mwenye kutumia Aayah ya “al-Maaidah”:

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ

“Ee Mtume! Fikisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako.” (05:67)

ya kwamba inahusiana na uongozi wa ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh)?

Jibu: Hizi ni tafsiri za Raafidhwah. Hapa Allaah (Ta´ala) anamzungumzisha Mtume. Raafidhwah wamemfanya Mtume kuwa ni ´Aliy. Yeye ndiye ambaye wamemfanya kuwa ni Mtume. Bali wamemfanya kuwa ni mungu na kwamba yeye ndiye ambaye anaendesha ulimwengu. Allaah (Ta´ala) anamzungumzisha Mtume:

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ

“Ee Mtume! Fikisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukufikisha ujumbe Wake. Na Allaah atakuhifadhi kutokamana na watu. Hakika Allaah haongoi watu makafiri.”

Mtume ni nani? Je, ni ´Aliy au ni Muhammad (Swalla Allaahu ´alayh wa sallam)? Amesema:

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ

“Ee Mtume! Fikisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukufikisha ujumbe Wake. Na Allaah atakuhifadhi kutokamana na watu. Hakika Allaah haongoi watu makafiri.”

Hakuna anayefasiri namna hiyo isipokuwa mtu ambaye moyoni mwake mna maradhi. Hapa Allaah anamzungumzisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na yeye anasema kuwa “Mtume” anayekusudiwa ni ´Aliy! Hii ni kufuru na ni kuritadi. Asiyeamini kuwa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndiye Mtume wa Allaah au akadai kuwa Jibriyl alitumwa kwa ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) na akawa amefanya khiyana na badala yake akamwendea Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), watu aina hii ukafiri na upotevu wao ni mbaya kabisa.

  • Mhusika: ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh al-Qaa´idah al-Marraakushiyyah (01)
  • Imechapishwa: 01/05/2020