Alikua hajui kama msikiti uko na kaburi

Swali: Niliswali kwenye msikiti mmoja ulio na kaburi swalah nyingi. Pindi nilipojua kwamba uko na kaburi nikaacha kuswali. Je, nizirudi upya zile swalah nilizoswali ndani yake?

Jibu: Ndio, zirudi zile swalah ulizoswali kwa sababu ni batili. Uliswali kwenye msikiti ulio na kaburi. Haijalishi kitu hata kama ulikuwa hujui. Punde tu baada ya kujua unatakiwa kuzirudi swalah zako, kwa sababu ni swalah zilizokatazwa na makatazo yanapelekea katika kuharibika.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (96) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/igahthat-12021440h.mp3
  • Imechapishwa: 23/05/2019