Swali: Mwanamke akiwaongoza wanawake katika Swalah, je, asimame mbele ya wanawake au asimame katikati yao kama alivyofanya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anha). Aliswalisha watu, akasimama katikati yao. Kasema hili Imaam al-Bayhaqiy? Je, hili limethibiti kwake? Na kama limethibiti, je inafaa kuitumia kama hoja?
Jibu: Ndio limethibiti. Na kuna upokezi mwingine unaofanana na wa ´Aaishah ya kwamba Ummu Salamah alifanya hivyo. Ingawa kitendo cha ´Aaishah na Ummu Salamah vimethibiti, lakini si hoja. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:
“Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”
Na Hadiyth hii inamgusa mwanaume na mwanamke. Kama ilivyo katika Kauli Yake (Ta´ala):
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ
“Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah.” (02:110)
Hii inamgusa mwanaume namwanamke. Lililo la dhahiri ni kuwa, Sunnah ni mwanamke atangulie mbele ya wanawake kama afanyavyo Imamu.
- Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=778
- Imechapishwa: 08/03/2018
Swali: Mwanamke akiwaongoza wanawake katika Swalah, je, asimame mbele ya wanawake au asimame katikati yao kama alivyofanya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anha). Aliswalisha watu, akasimama katikati yao. Kasema hili Imaam al-Bayhaqiy? Je, hili limethibiti kwake? Na kama limethibiti, je inafaa kuitumia kama hoja?
Jibu: Ndio limethibiti. Na kuna upokezi mwingine unaofanana na wa ´Aaishah ya kwamba Ummu Salamah alifanya hivyo. Ingawa kitendo cha ´Aaishah na Ummu Salamah vimethibiti, lakini si hoja. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:
“Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”
Na Hadiyth hii inamgusa mwanaume na mwanamke. Kama ilivyo katika Kauli Yake (Ta´ala):
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ
“Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah.” (02:110)
Hii inamgusa mwanaume namwanamke. Lililo la dhahiri ni kuwa, Sunnah ni mwanamke atangulie mbele ya wanawake kama afanyavyo Imamu.
Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=778
Imechapishwa: 08/03/2018
https://firqatunnajia.com/al-waadiiy-kuhusu-mwanamke-kuwa-mbele-anapowaongoza-wenzio-katika-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)