al-Fawzaan kuwatibu wenye kutumia madawa ya kulevya

Swali: Mtu anakuwa katika aina ya watu gani ikiwa wendawazimu wake ni kwa kujisababishia mwenyewe kama vile kumuasi Allaah wale ambao wanatumia madawa ya kulevya ambapo wakawa wendawazimu kwa sababu ya madawa haya?

Jibu: Huyu sio mwendawazimu. Huyu madawa ya kulevya ndio yamemuathiri kwenye ubongo wake. Sio mwendawazimu. Huyu anapata dhambi kwa kitendo chake. Kwa kuwa amejifanyia vibaya mwenyewe.

Leo kuna dawa ambapo wanawatibu wale walipewa mtihani kwa vitu kama hivi. Kuna ambao wanapona na wanapata fahamu. Midhali kuna dawa watibiwe.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Furqaan (10) http://alfawzan.af.org.sa/node/2053
  • Imechapishwa: 16/01/2017