Miongoni mwa Bid´ah hizo ni Bid´ah ya mazazi ya Mtume. Kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni jambo la wajibu kwa kila muislamu. Imani ya muislamu haitimii mpaka Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) awe ni mwenye kupendwa zaidi kwake kuliko anavyojipenda mwenyewe, mtoto wake, baba yake na watu wote kwa jumla. Haya yamepokelewa katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy.
Lakini hata hivyo kumpenda kunakuwa kwa kumtii na kumfuata. Kwa msemo mwingine ni kwa kutekeleza maamrisho yake na kujiepusha na makatazo yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Amekataza Bid´ah bali na kuitahadharisha pale aliposema:
“Kila Bid´ah ni upotevu.”
“Atakayetenda kitendo ambacho hamna ndani yake dini yetu, basi atarudishiwa mwenyewe.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Haikuthibiti kwake yeye, makhaliyfah wake, Maswahabah zake na wale wanachuoni wenye kustahiki kufuatwa yeyote ambaye alifanya maulidi. Uhakika wa mambo ni kwamba maulidi haya yalizushwa na al-Faatwimiyyuun al-´Ubaydiyyuun ambao walikuwa ni Raafidhwah. Wanajinasibisha na Faatwimah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ilihali uhakika wa mambo walikuwa ni mayahudi.
- Mhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Bid´ah – Dhwawaabitwuhaa wa atharuhaa as-Sayyiu´ fiyl-Ummah, uk. 18
- Imechapishwa: 27/08/2020
Miongoni mwa Bid´ah hizo ni Bid´ah ya mazazi ya Mtume. Kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni jambo la wajibu kwa kila muislamu. Imani ya muislamu haitimii mpaka Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) awe ni mwenye kupendwa zaidi kwake kuliko anavyojipenda mwenyewe, mtoto wake, baba yake na watu wote kwa jumla. Haya yamepokelewa katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy.
Lakini hata hivyo kumpenda kunakuwa kwa kumtii na kumfuata. Kwa msemo mwingine ni kwa kutekeleza maamrisho yake na kujiepusha na makatazo yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Amekataza Bid´ah bali na kuitahadharisha pale aliposema:
“Kila Bid´ah ni upotevu.”
“Atakayetenda kitendo ambacho hamna ndani yake dini yetu, basi atarudishiwa mwenyewe.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Haikuthibiti kwake yeye, makhaliyfah wake, Maswahabah zake na wale wanachuoni wenye kustahiki kufuatwa yeyote ambaye alifanya maulidi. Uhakika wa mambo ni kwamba maulidi haya yalizushwa na al-Faatwimiyyuun al-´Ubaydiyyuun ambao walikuwa ni Raafidhwah. Wanajinasibisha na Faatwimah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ilihali uhakika wa mambo walikuwa ni mayahudi.
Mhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Bid´ah – Dhwawaabitwuhaa wa atharuhaa as-Sayyiu´ fiyl-Ummah, uk. 18
Imechapishwa: 27/08/2020
https://firqatunnajia.com/al-faqiyhiy-kuhusu-maulidi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)