Swali: Ni ipi hukumu ya Qaz´?
Jibu: Qaz´ ni kunyoa sehemu ya kichwa na kuacha sehemu nyingine. Imegawanyika aina mbalimbali:
Ya kwanza: Akanyoa sehemu ya kichwa pasi na kupangilia. Kwa mfano akanyoa upande wa kulia, kwenye kona na upande wa kushooto.
Ya pili: Akanyoa katikati ya kichwa na akaacha upande wake.
Ya tatu: Akanyoa upande wa kichwa na akaacha katikati yake. Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:
“Hivyo ndivyo wanavyofanya wapumbavu.”
Ya nne: Mtu akanyoa kwenye kona na akaacha zilizobaki.
Qaz´ aina zote hizi imechukizwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuona kijana aliyenyoa sehemu ya kichwa chake tu ambapo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamuamrisha ima azinyoa zote au aziache zote. Lakini hata hivyo ikiwa Qaz´ ni yenye kufanana na makafiri inakuwa haramu. Kwa sababu imeharamishwa kwa mtu kujifananisha na makafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni katika wao.”
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/118)
- Imechapishwa: 28/06/2017
Swali: Ni ipi hukumu ya Qaz´?
Jibu: Qaz´ ni kunyoa sehemu ya kichwa na kuacha sehemu nyingine. Imegawanyika aina mbalimbali:
Ya kwanza: Akanyoa sehemu ya kichwa pasi na kupangilia. Kwa mfano akanyoa upande wa kulia, kwenye kona na upande wa kushooto.
Ya pili: Akanyoa katikati ya kichwa na akaacha upande wake.
Ya tatu: Akanyoa upande wa kichwa na akaacha katikati yake. Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:
“Hivyo ndivyo wanavyofanya wapumbavu.”
Ya nne: Mtu akanyoa kwenye kona na akaacha zilizobaki.
Qaz´ aina zote hizi imechukizwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuona kijana aliyenyoa sehemu ya kichwa chake tu ambapo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamuamrisha ima azinyoa zote au aziache zote. Lakini hata hivyo ikiwa Qaz´ ni yenye kufanana na makafiri inakuwa haramu. Kwa sababu imeharamishwa kwa mtu kujifananisha na makafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni katika wao.”
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/118)
Imechapishwa: 28/06/2017
https://firqatunnajia.com/aina-mbalimbali-za-qaz-na-hukumu-zake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)