Hapa mwandishi ametaja aina sita ya dalili zinazoonesha kuwa Allaah yuko juu ya viumbe Wake. Ibn-ul-Qayyim yeye ametaja karibu aina ishirini na moja njia miongoni mwa njia za kunukuu zenye kuonyesha kuwa Allaah (Subhaanah) yuko juu ya mbingu na juu ya ´Arshi. Ameyataja hayo katika “Kaafiyat-ush-Shaafiyah” . Dalili zote hizi Jahmiyyah na Mu´tazilah wamezipuuzia mbali na wakapinga kuwa Allaah yuko juu ya ´Arshi. Wamesema kuwa Allaah amechanganyika na viumbe Wake – tunaomba kinga kwa Allaah.

Ashaa´irah waliotangulia walikuwa wakithibitisha Ujuu. Uhakika wa mambo ni kwamba imethibiti kutoka kwa Abul-Hasan al-Ash´ariy na Ibn Kullaab wakithibitisha Ujuu. Lakini Ashaa´irah waliokuja nyuma na wale wajinga wakawa ni wenye kuafikiana na Jahmiyyah katika kukanusha Ujuu. Wanafasiri Ujuu kwamba ni uwezo na nguvu. Wote hawa wamekanusha Ujuu na wamezitupilia mbali dalili za Qur-aan na Sunnah kuhusu Ujuu.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh al-Qaa´idah al-Marraakushiyyah, uk. 45
  • Imechapishwa: 30/04/2020