Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kufanya liwati?

Jibu: Shaykh Ibraahiym na wanachuoni wengine wametaja kwamba mwenye kufanya ushoga ni yule anayemwendea mwanaume. Kumwingilia mwanaume ni ushoga. Allaah amelikemea hilo na amebainisha jambo la ushoga katika kisa cha watu wa Luutw. Allaah aliwaangamiza wote na akateketeza mji wao kwa kuupindua juu chini. Kisha baada ya hapo akawateremshia mvua ya mawe ya udongo uliokokwa.

al-Waliyd bin ´Abdil-Malik, ambaye alikuwa ni kiongozi wa waumini, amesema:

”Kama Allaah asingelitaja kisa cha mashoga katika Qur-aan, basi nisingeliamini kama mwanaume kweli anaweza kumwendea mwanaume mwenzie.”

Ni uchafu wenye kufedhehi. Ni mchafu na mbaya zaidi kuliko hata uzinzi. Kwa ajili hii ndio maana hukumu yake imekuja kwamba ni kuuawa. Haya ndio maoni ya Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wote (Radhiya Allaahu ´anhum) wameafikiana kwamba mashoga wanatakiwa kuuawa kabisa. Ni mamoja mashoga hao bado hawajaingia katika ndoa au tayari wameshaingia katika ndoa. Baadhi ya wanachoni wanaonelea kwamba ni kama mzinifu ambapo wanaonelea kwamba yule ambaye kishaingia katika ndoa basi anatakiwa kupigwa mawe na yule ambaye hajaingia ndani ya ndoa basi anatakiwa kupigwa bakora mia na kufukuzwa mbali na mji kwa muda wa mwaka. Lakini hata hivyo haya ni maoni dhaifu. Maoni sahihi ni kwamba mashoga wanatakiwa kuuawa. Haya ndio maoni ya sawa. Anatakiwa kuuawa. Ni mamoja auawe kwa upanga au kwa apigwe mawe kama mzinifu ambaye ameshaoa.

Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wameafikiana juu ya kuuawa kwao. Lakini baadhi yao wameonelea kwamba anatakiwa kupigwa mawe kama anavyopigwa mawe mzinifu ambaye kishaingia katika ndoa. Wengine wameonelea kwamba wanatakiwa kutupwa kutoka juu ya mlima mrefu. Baadhi ya wengine wameonelea kwamba wanatakiwa kuchomwa moto. Lakini maoni ya sawa juu ya hili ni kwamba wanatakiwa kuuawa kwa upanga kama ilivyokuja katika Hadiyth kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:

”Mtakayempata anafanya kitendo cha ushoga/liwati, basi muueni yule mwenye kufanya na yule mwenye kufanywa.”

Cheni ya wapokezi wa Hadiyth hii haina neno japokuwa ina baadhi ya tofauti. Lakini hata hivyo inasapotiwa na kutiwa nguvu na maafikiano ya Maswahabah.

Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wameafikiana juu ya kuuawa kwao. Mashoga wanatakiwa kuuawa pasi na kipingamizi. Ni mamoja aliwahi kuingia katika ndoa au bado. Walichotofautiana ni ile namna ya kuuawa kwao; je, auawe kwa kuchomwa moto, kupigwa mawe au kwa kupigwa upanga? Maoni ya sawa ni kwamba auwawe kwa kupigwa upanga. Kwa sababu hairuhusiwi kuadhibu kwa moto isipokuwa Allaah peke yake. Kadhalika suala la kupigwa mawe limethibiti kwa mzinifu ambaye ameshaoa au kuolewa. Kwa hivyo asilinganishwe juu yake shoga, kwani yeye suala lake ni jengine. Lakini hata hivyo anatakiwa kuuawa kwa kupigwa upanga. Inahusiana na wote wawili; mwenye kufanya na mwenye kufanyiwa. Hapa ni pale ambapo ´ibaadah itakuwa ni yenye kuwawajibikia. Hili ni kutokana na uchafu wa dhambi yao na fedheha yao kubwa. Ni wajibu kulikimbia jambo hilo na kulitahadharisha. Kwa hivyo kuuawa ni jambo stahiki nafasi kama hii kwa ajili ya kutahadharisha juu ya uchafu na fedheha hii kubwa na mbaya.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1727/%D8%AD%D8%AF-%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%88%D8%A7%D8%B7
  • Imechapishwa: 04/11/2018