Swali: Ami yake Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakupatapo kuingia katika Uislamu na akafa juu ya ukafiri, pamoja na kutangaa kwake waziwazi juu ya kumtetea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Je, haya yanaingia ndani ya Hadiyth:
“Hakika mmoja wenu atafanya matendo ya watu wa Peponi kwa yale yanayowadhihirikia watu… “?
Jibu: Alifanya hivo kwa sababu ya ule udugu, kama ilivyotajwa katika maneno Yake (Ta´ala):
إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ
”Hakika wewe huwezi kumwongoza umpendaye lakini Allaah ndiye anamwongoza mtakaye.”[1]
Abu Twaalib akasema:
“Lau kama si kutukanywa na Quraysh, basi ningeliitamka.”
Bi maana ningeliitamka shahaadah.
Ibn Hishaam ameeleza katika wasifu wake kwamba al-´Abbaas amesimulia kuwa alitamka shahaadah, lakini katika kipindi hicho alikuwa bado hajasilimu na hivyo upokezi wake si wenye kukubaliwa. Kuhusu maneno yake:
Nilijua kuwa dini ya Muhammad
ndio dini bora ya viumbe
Isingekuwa kwa ajili ya lawama na kuogopwa kutukanywa
basi ungeniona ni mwenye kufunguka waziwazi na kukubali[2]
hayapelekei kwamba aliingia katika Uislamu. Alikataa kuingia katika Uislamu, kama ambavo al-Bukhaariy na Muslim walivyopokea kutoka kwa al-Musayyab bin Huzn. Ndugu yetu Qaasim bin ´Abdillaah at-Ta´ziy ametunga kitabu chenye thamani sana ambapo amemraddi Dahlaan kwa jina ”Asnaa al-Matwaalib fiy Islaam Abiy Twaalib”.
[1] 28:56
[2] al-Bidaayah wan-Nihaayah (3/42).
- Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1337
- Imechapishwa: 22/02/2020
Swali: Ami yake Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakupatapo kuingia katika Uislamu na akafa juu ya ukafiri, pamoja na kutangaa kwake waziwazi juu ya kumtetea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Je, haya yanaingia ndani ya Hadiyth:
“Hakika mmoja wenu atafanya matendo ya watu wa Peponi kwa yale yanayowadhihirikia watu… “?
Jibu: Alifanya hivo kwa sababu ya ule udugu, kama ilivyotajwa katika maneno Yake (Ta´ala):
إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ
”Hakika wewe huwezi kumwongoza umpendaye lakini Allaah ndiye anamwongoza mtakaye.”[1]
Abu Twaalib akasema:
“Lau kama si kutukanywa na Quraysh, basi ningeliitamka.”
Bi maana ningeliitamka shahaadah.
Ibn Hishaam ameeleza katika wasifu wake kwamba al-´Abbaas amesimulia kuwa alitamka shahaadah, lakini katika kipindi hicho alikuwa bado hajasilimu na hivyo upokezi wake si wenye kukubaliwa. Kuhusu maneno yake:
Nilijua kuwa dini ya Muhammad
ndio dini bora ya viumbe
Isingekuwa kwa ajili ya lawama na kuogopwa kutukanywa
basi ungeniona ni mwenye kufunguka waziwazi na kukubali[2]
hayapelekei kwamba aliingia katika Uislamu. Alikataa kuingia katika Uislamu, kama ambavo al-Bukhaariy na Muslim walivyopokea kutoka kwa al-Musayyab bin Huzn. Ndugu yetu Qaasim bin ´Abdillaah at-Ta´ziy ametunga kitabu chenye thamani sana ambapo amemraddi Dahlaan kwa jina ”Asnaa al-Matwaalib fiy Islaam Abiy Twaalib”.
[1] 28:56
[2] al-Bidaayah wan-Nihaayah (3/42).
Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1337
Imechapishwa: 22/02/2020
https://firqatunnajia.com/abu-twaalib-hakuingia-ndani-ya-uislamu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)