Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimsikia mtu akiomba ndani ya swalah yake pasi na kumtukuza Allaah (Ta´ala) na wala hakumsifu yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akasema: “Amefanya haraka.” Kisha akamwita na akamwambia yeye na wengine:
“Pindi mmoja wenu anaposwali basi aanze kwanza kumhimidi na kumsifu Mola wake (Jalla wa ´Azz). Halafu amsifu Mtume na kisha baada ya hapo aombe anachotaka.”[1]
Alimsikia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mtu mmoja anaswali akamtukuza na kumshukuru na kumsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akasema:
“Omba utaitikiwa. Uliza utapewa.”[2]
[1] Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Khuzaymah (2/83/1) na al-Haakim ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
Tambua kwamba Hadiyth hii ni dalili inayoonyesha kuwa ni wajibu kumsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Tashahhud hii. Haya ndio maoni ya ash-Shaafi´iy na Ahmad katika maoni yake ya mwisho yaliyopokelewa kwake. Kabla yao walikuwa na maoni tofauti kutoka kwa kundi la Maswahabah. Bali al-Ajurriy amesema:
“Yule asiyemsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Tashahhud yake ya mwisho basi ni wajibu kwake kuirudi swalah yake.” (ash-Shariy´ah, uk. 415).
Kwa ajili hiyo ni dhuluma kumtuhumu ash-Shaafi´iy kwamba amepondoka katika suala hili kwa vile anaonelea kuwa kitendo hicho ni wajibu, kama alivyobainisha Faqiyh al-Haytamiy katika ”ad-Durr al-Mandhuud fiys-Swalaati was-Salaami ´alaa Swaahib-il-Maqaam al-Mahmuud” (13-16).
[2] an-Nasaa’iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 158-159
- Imechapishwa: 08/01/2019
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimsikia mtu akiomba ndani ya swalah yake pasi na kumtukuza Allaah (Ta´ala) na wala hakumsifu yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akasema: “Amefanya haraka.” Kisha akamwita na akamwambia yeye na wengine:
“Pindi mmoja wenu anaposwali basi aanze kwanza kumhimidi na kumsifu Mola wake (Jalla wa ´Azz). Halafu amsifu Mtume na kisha baada ya hapo aombe anachotaka.”[1]
Alimsikia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mtu mmoja anaswali akamtukuza na kumshukuru na kumsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akasema:
“Omba utaitikiwa. Uliza utapewa.”[2]
[1] Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Khuzaymah (2/83/1) na al-Haakim ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
Tambua kwamba Hadiyth hii ni dalili inayoonyesha kuwa ni wajibu kumsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Tashahhud hii. Haya ndio maoni ya ash-Shaafi´iy na Ahmad katika maoni yake ya mwisho yaliyopokelewa kwake. Kabla yao walikuwa na maoni tofauti kutoka kwa kundi la Maswahabah. Bali al-Ajurriy amesema:
“Yule asiyemsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Tashahhud yake ya mwisho basi ni wajibu kwake kuirudi swalah yake.” (ash-Shariy´ah, uk. 415).
Kwa ajili hiyo ni dhuluma kumtuhumu ash-Shaafi´iy kwamba amepondoka katika suala hili kwa vile anaonelea kuwa kitendo hicho ni wajibu, kama alivyobainisha Faqiyh al-Haytamiy katika ”ad-Durr al-Mandhuud fiys-Swalaati was-Salaami ´alaa Swaahib-il-Maqaam al-Mahmuud” (13-16).
[2] an-Nasaa’iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 158-159
Imechapishwa: 08/01/2019
https://firqatunnajia.com/96-uwajibu-wa-kumswalia-mtume/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)