Swali 92: Tunawaona watu wengi baada ya kumzika maiti wanalinyanyua kaburi lake zaidi ya shibiri. Ninapowakataza wanasema kuwa wanafanya hivo kwa ajili ya kumlinda kutokamana na mafuriko. Vivyo hivyo nawaona kuwa wanazidisha changarawe juu ya kaburi baada ya kumzika zaidi ya ule udongo wake uliotoka ndani. Vivyo hivyo wananyunyizia juu yake maji. Ni ipi hukumu ya matendo yao[1]?
Jibu: Yote haya hayana neno. Bora ni shibiri moja na mfano wake. Wakizidisha kidogo kwa changarawe au mfano wake jambo ni lenye wasaa. Ili makaburi yatambulike na yasitweze. Wakimfukia kwa udongo wake na wakaweka juu yake changarawe na wakanyanyuzia maji ili udongo ukae imara, yote haya hayana neno. Kwa sababu kufanya hivo kunalinda udongo wake na kufanya ubaki.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/208-209).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 64-65
- Imechapishwa: 06/01/2022
Swali 92: Tunawaona watu wengi baada ya kumzika maiti wanalinyanyua kaburi lake zaidi ya shibiri. Ninapowakataza wanasema kuwa wanafanya hivo kwa ajili ya kumlinda kutokamana na mafuriko. Vivyo hivyo nawaona kuwa wanazidisha changarawe juu ya kaburi baada ya kumzika zaidi ya ule udongo wake uliotoka ndani. Vivyo hivyo wananyunyizia juu yake maji. Ni ipi hukumu ya matendo yao[1]?
Jibu: Yote haya hayana neno. Bora ni shibiri moja na mfano wake. Wakizidisha kidogo kwa changarawe au mfano wake jambo ni lenye wasaa. Ili makaburi yatambulike na yasitweze. Wakimfukia kwa udongo wake na wakaweka juu yake changarawe na wakanyanyuzia maji ili udongo ukae imara, yote haya hayana neno. Kwa sababu kufanya hivo kunalinda udongo wake na kufanya ubaki.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/208-209).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 64-65
Imechapishwa: 06/01/2022
https://firqatunnajia.com/92-bora-ni-kaburi-linyanyuke-juu-ya-ardhi-kwa-kiasi-cha-shibiri/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)