91. al-Qummiy upotoshaji wake wa nane wa an-Nisaa´

al-Qummiy amesema pindi alipokuwa akifasiri Aayah:

وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذ ظَّلَمُوا أَنفُسَهُمْ جَاءُوكَ فَاسْتَغْفَرُوا اللَّـهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّـهَ تَوَّابًا رَّحِيمًا

“Na lau wao pale walipojidhulumu nafsi zao wangelikujia wakamuomba Allaah msamaha na Mtume akawaombea msamaha, basi wangelimkuta Allaah ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu.”[1]

“Baba yangu amenihadithia, kutoka kwa Ibn Abiy ´Umayr, kutoka kwa Ibn Udhaynah, kutoka kwa Zaraarah, kutoka kwa Abu Ja´far aliyesema: “Imeteremshwa namna hii:

وَلَوْ أَنَّهُمْ إِذ ظَّلَمُوا أَنفُسَهُمْ جَاءُوكَ يا علي فَاسْتَغْفَرُوا اللَّـهَ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمُ الرَّسُولُ لَوَجَدُوا اللَّـهَ تَوَّابًا رَّحِيمًا

“Na lau wao pale walipojidhulumu nafsi zao wangelikujia, ee ´Aliy, wakamuomba Allaah msamaha na Mtume akawaombea msamaha, basi wangelimkuta Allaah ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu.”

Maadui wa Allaah wamemsemea uongo Abu Ja´far as-Swadiyq. Hakuna uwezekano wowote kabisa kwamba angelimzulia uongo Allaah tafsiri hii na nyongeza hii katika Qur-aan. Huu ni katika uzushi wa maadui wa Allaah Baatwiniyyah kwa ajili ya kutaka kuitukana Qur-aan na kudai kuwa haikuhifadhiwa na kuwatuhumu Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba ni makhaini wenye kuongeza na kupunguza katika Qur-aan vile wanavotaka. Ni mara ngapi Raafidhwah hawa wameipotosha Qur-aan! Ni mara ngapi wamewazulia uongo Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuwatuhumu ukafiri!

[1] Tafsiyr al-Qummiy (1/142).

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intisaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 136
  • Imechapishwa: 23/11/2017