9. Allaah ameizuia tawbah kwa mtu wa Bid´ah

Yamepokelewa katika Hadiyth ya Anas bin Maalik pamoja na al-Hasan al-Baswriy kwa mfuatano wa wasimulizi uliokatika kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ibn Wadhdhwaah ameeleza kuwa Ayyuub amesema:

“Kuna mtu katika sisi aliyekuwa na ´Aqiydah mbovu na baadae akaiacha. Nikamwendea Muhammad bin Siriyn na kumwambia: “Je, unajua kuwa fulani ameacha ´Aqiydah yake?” Akasema: “Tazama amegeuka kuwa nini. Sehemu ya mwisho ya Hadiyth pigo zaidi kwao kuliko sehemu yake ya mwanzo:

“Wanatoka nje ya Uislamu kisha hawarudi tena.”[1]

Ahmad bin Hanbal aliulizwa maana yake akajibu:

“Hawawafikishwi kutubu.”

[1] Muslim (1067).

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwl-ul-Islaam, uk. 28-29
  • Imechapishwa: 23/10/2016