Swali 89: Imepokelewa katika Hadiyth juu ya maamrisho ya kumwombea du´aa maiti  baada ya kuzikwa kwake. Je, amri hii ni kwa njia ya ulazima au imependekezwa tu? Tumeona kuwa watu wameacha Sunnah hii au wajibu huu baada ya kumzika maiti[1]?

Jibu: Kumwombea du´aa ya uthabiti na msamaha maiti baada ya kuzikwa ni jambo limependekezwa na sio lazima. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anapomaliza kumzika maiti basi husimama karibu naye na kusema:

“Mwombeeni msamaha ndugu yenu na mtakieni uimara; kwani hakika hivi sasa anahojiwa.”[2]

[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/205).

[2] Abu Daawuud (3221).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 63
  • Imechapishwa: 04/01/2022