23- Muslim amepokea kupitia kwa Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba kuna watu wa Answaar walimuomba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawapa, wakamuomba [tena] akawapa mpaka kile alichokuwa nacho kikaisha. Akasema:
“Sintokuwa na mali nikaacha kuwapa. Mwenye kutaka utakaso basi Allaah atamtakasa. Mwenye kutafuta utajiri basi Allaah atamtajirisha. Mwenye kutaka uoni wa mbali [baswiyrah] basi Allaah atamfanya awe hivo. Hakuna aliepewa zawadi bora na ilio kuvunjufu zaidi kuliko subira.”[1]
24- Wanachuoni wetu (Rahimahumu Allaah) wamesema “Mwenye kutaka utakaso” bi maana kusubiri. Miongoni mwa hayo ni Kauli ya Allaah (Ta´ala):
وَلْيَسْتَعْفِفِ الَّذِينَ لَا يَجِدُونَ نِكَاحًا حَتَّىٰ يُغْنِيَهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ
“Na wajizuilie na uchafu wale wasiopata chakutolea, mpaka Allaah Awatajirishe kwa fadhila Zake.” (24:33)
Ibn ´Arafah na watu wengine wa lugha wamesema:
“Basi na asubiri.”
Maana yake ni kwamba yule mwenye kusubiri na kuacha kuwaomba watu kitu basi Allaah atamtakasa uso wake na kumwondoshea ufukara wake.
“Mwenye kutafuta utajiri… ” – bi maana kutoka kwa Allaah.
“… basi Allaah atamtajirisha” – bi maana atautajirisha moyo wake au atampa na kuacha kuwategemea viumbe. Inawezekana vilevile Allaah akamtukuza mtu huyo na kumpa yote mawili.
25- Ibn Abiyd-Dunyaa amepokea kuwa Bakr bin ´Abdillaah akisema katika du´aa yake:
“Ee Allaah! Turuzuku kunakofadhila Zako ambazo zitatufanya kukushukuru zaidi na kukutegemea Wewe zaidi na kutowategemea wengine wote.”
[1] al-Bukhaariy (03/335) na Muslim (02/729).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 28-29
- Imechapishwa: 18/03/2017
23- Muslim amepokea kupitia kwa Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba kuna watu wa Answaar walimuomba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawapa, wakamuomba [tena] akawapa mpaka kile alichokuwa nacho kikaisha. Akasema:
“Sintokuwa na mali nikaacha kuwapa. Mwenye kutaka utakaso basi Allaah atamtakasa. Mwenye kutafuta utajiri basi Allaah atamtajirisha. Mwenye kutaka uoni wa mbali [baswiyrah] basi Allaah atamfanya awe hivo. Hakuna aliepewa zawadi bora na ilio kuvunjufu zaidi kuliko subira.”[1]
24- Wanachuoni wetu (Rahimahumu Allaah) wamesema “Mwenye kutaka utakaso” bi maana kusubiri. Miongoni mwa hayo ni Kauli ya Allaah (Ta´ala):
وَلْيَسْتَعْفِفِ الَّذِينَ لَا يَجِدُونَ نِكَاحًا حَتَّىٰ يُغْنِيَهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ
“Na wajizuilie na uchafu wale wasiopata chakutolea, mpaka Allaah Awatajirishe kwa fadhila Zake.” (24:33)
Ibn ´Arafah na watu wengine wa lugha wamesema:
“Basi na asubiri.”
Maana yake ni kwamba yule mwenye kusubiri na kuacha kuwaomba watu kitu basi Allaah atamtakasa uso wake na kumwondoshea ufukara wake.
“Mwenye kutafuta utajiri… ” – bi maana kutoka kwa Allaah.
“… basi Allaah atamtajirisha” – bi maana atautajirisha moyo wake au atampa na kuacha kuwategemea viumbe. Inawezekana vilevile Allaah akamtukuza mtu huyo na kumpa yote mawili.
25- Ibn Abiyd-Dunyaa amepokea kuwa Bakr bin ´Abdillaah akisema katika du´aa yake:
“Ee Allaah! Turuzuku kunakofadhila Zako ambazo zitatufanya kukushukuru zaidi na kukutegemea Wewe zaidi na kutowategemea wengine wote.”
[1] al-Bukhaariy (03/335) na Muslim (02/729).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 28-29
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/8-mwenye-kutafuta-utajiri-basi-allaah-atamtajirisha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)