Swali 76: Swalah ya mtu inaharibika akizungumza ndani ya swalah kwa kusahau?
Jibu: Akizungumza muislamu ndani ya swalah kwa kusahau au kwa ujinga swalah yake haibatiliki. Ni mamoja swalah hiyo ni ya faradhi au ya iliyopendekezwa. Allaah (Subhaanah) amesema:
رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Ee Mola wetu! Usituchukulie pale tutaposahau au tukikosea.”[1]
Imethibiti katika “as-Swahiyh” kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Nimekwishafanya.”
Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa Mu´aawiyah bin al-Hakam as-Sulamiy (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba alimtakia rehema mchemuaji ndani ya swalah kutokana na kujahili kwake hukumu ya ki-Shari´ah ambapo walioko pambizoni mwake wakamkemea kwa kumwashiria. Baadaye akamuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya hilo na hakumwamrisha kuirudia swalah yake. Msahaulifu ni kama mfano wa mjinga na aula zaidi. Jengine ni kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alizungumza ndani ya swalah kwa kusahau na hakuirudia swalah yake. Bali alikamilisha swalah yake kama ilivyopokelewa katika Hadiyth Swahiyh kupitia kwa Ibn Mas´uud, ´Imraan bin Huswayn na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh).
Kuhusu kuashiria ndani ya swalah hapana neno ikiwa haja imepelekea kufanya hivo.
[1] 02:286
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 81
- Imechapishwa: 22/09/2022
Swali 76: Swalah ya mtu inaharibika akizungumza ndani ya swalah kwa kusahau?
Jibu: Akizungumza muislamu ndani ya swalah kwa kusahau au kwa ujinga swalah yake haibatiliki. Ni mamoja swalah hiyo ni ya faradhi au ya iliyopendekezwa. Allaah (Subhaanah) amesema:
رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Ee Mola wetu! Usituchukulie pale tutaposahau au tukikosea.”[1]
Imethibiti katika “as-Swahiyh” kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amesema:
“Nimekwishafanya.”
Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” yake kupitia kwa Mu´aawiyah bin al-Hakam as-Sulamiy (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba alimtakia rehema mchemuaji ndani ya swalah kutokana na kujahili kwake hukumu ya ki-Shari´ah ambapo walioko pambizoni mwake wakamkemea kwa kumwashiria. Baadaye akamuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya hilo na hakumwamrisha kuirudia swalah yake. Msahaulifu ni kama mfano wa mjinga na aula zaidi. Jengine ni kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alizungumza ndani ya swalah kwa kusahau na hakuirudia swalah yake. Bali alikamilisha swalah yake kama ilivyopokelewa katika Hadiyth Swahiyh kupitia kwa Ibn Mas´uud, ´Imraan bin Huswayn na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh).
Kuhusu kuashiria ndani ya swalah hapana neno ikiwa haja imepelekea kufanya hivo.
[1] 02:286
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Muhimmah, uk. 81
Imechapishwa: 22/09/2022
https://firqatunnajia.com/76-amesahau-akazungumza-ndani-ya-swalah-kwa-kusahau/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)