74. al-´Ayyaashiy upotoshaji wake wa kumi na mbili wa Aal ´Imraan

al-´Ayyaashiy amesema pindi alipokuwa akifasiri Aayah:

وَمَا مُحَمَّدٌ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ ۚ أَفَإِن مَّاتَ أَوْ قُتِلَ انقَلَبْتُمْ عَلَىٰ أَعْقَابِكُمْ

“Muhammad si chochote isipokuwa ni Mtume tu [na] wamekwishapita kabla yake Mitume [wengine]. Je, akifa au akiuawa mtageuka nyuma ya visigino vyenu?”[1]

“al-Husayn bin Mundhir amesema: “Nilimuuliza Abu ´Abdillaah: “Alikufa au aliuawa?” Akasema: “Anamaanisha Maswahabah zake ambao walifanya ya kufanya.”[2]

Raafidhwah Baatwiniyyah wanamaanisha kuwa Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndio ambao walimuua.

Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambao walijitolea mali na nafsi zao na ambao walikuwa wanampenda zaidi kuliko wanavyojipenda mwenyewe, baba zao, watoto wao, ndugu zao, jamaa zao na mali zao ndio ambao walikuwa maadui wake kwa mtazamo wa viumbe wadhalilifu, waongo, wafanya khiyana na walaghai wakubwa kabisa wa Allaah dhidi ya Uislamu, waislamu na familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Sambamba na hilo Raafidhwah hawa – ambao ndio warithi wa mayahudi na waabudu moto – ndio wanaompenda, kusimama upande wake na walio na wivu juu yake? Si mayahudi wala wengine hawawezi kufikia kufanya kama wanavyofanya Raafidhwah.

Allaah amewatakasa Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Aayah nyingi ikiwa ni pamoja vilevile na:

مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّـهِ ۚ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ ۖتَرَاهُمْ رُكَّعًا سُجَّدًا يَبْتَغُونَ فَضْلًا مِّنَ اللَّـهِ وَرِضْوَانًا ۖ سِيمَاهُمْ فِي وُجُوهِهِم مِّنْ أَثَرِ السُّجُودِ ۚ ذَٰلِكَ مَثَلُهُمْ فِي التَّوْرَاةِ ۚ وَمَثَلُهُمْ فِي الْإِنجِيلِ كَزَرْعٍ أَخْرَجَ شَطْأَهُ فَآزَرَهُ فَاسْتَغْلَظَ فَاسْتَوَىٰ عَلَىٰ سُوقِهِ يُعْجِبُ الزُّرَّاعَ لِيَغِيظَ بِهِمُ الْكُفَّارَ ۗ وَعَدَ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ مِنْهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا

“Muhammad ni Mtume wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi dhidi ya makafiri wanahurumiana baina yao. Utawaona wakirukuu na wakisujudu wakitafuta fadhila na radhi kutoka kwa Allaah. Alama zao dhahiri zi katika nyuso zao kutokana na athari za sujudu. Huo ni mfano wao katika Tawraat na mfano wao katika Injiyl kama mmea umetoa chipukizi lake, likautia nguvu kisha likawa nene, kisha likasimama sawasawa juu ya shina lake liwapendezeshe wakulima ili liwaghadhibishe makafiri. Allaah amewaahidi wale walioamini na wakatenda mema katika jinsia yao maghfirah na ujira mkubwa.”[3]

Huu ni ushahidi wa Allaah juu yao katika Tawraat, Injiyl na Qur-aan ukiwaraddi maadui wa Allaah ambao wanakasirika pale tu wanapotajwa Maswahabah wa Muhamamd (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na sifa zao ambazo Allaah amewatunuku. Watu hawa ni makafiri kwa mujibu wa ushahidi wa Allaah dhidi yao. Kwa sababu hakuna wanaowachukia sana Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama wao!

[1] 03:144

[2] Tafsiyr al-´Ayyaashiy (1/200).

[3] 48:29

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 113-114
  • Imechapishwa: 13/04/2017