Hakika baadhi ya wanawake na wasimamizi wao wanachukulia wepesi kwa aina mbalimbali za ukaaji faragha ikiwa ni pamoja na:
a) Mwanamke kukaa faragha pamoja na ndugu zake mume pamoja na kuacha wazi uso wake mbele yao. Faragha hii ina khatari zaidi kuliko nyingine. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Tahadharini na kuingia sehemu za wanawake.” Mtu mmoja katika Answaar akasema: “Ee Mtume wa Allaah! Unasemaje kuhusu al-Hamuu.” Akajibu: “al-Hamuu ni kifo.”
Ameipokea Ahmad, al-Bukhaariy, at-Tirmidhiy na akaisahihisha.
Maana ya al-Hamuu ni yule ndugu yake mume. Kama kwamba alichukia kukaa naye faragha. al-Haafidhw bin Hajar amesema katika “Fath-ul-Baariy”:
“Wanachuoni wa lugha wameafikiana juu ya kwamba al-Ahmaa´ (mashemeji) ni wale ndugu zake mume wa mke; kama baba yake mume, kaka yake mume, mtoto wa kaka yake, mabinamu na mfano wao.” Akasema tena: “Makusudio katika Hadiyth ni wale ndugu zake mume – mbali na wale baba zake na watoto wake; kwa sababu hao ni Mahram zake mke na inafaa kwao kukaa naye faragha na hawaitwi kuwa ni kifo – kimazowea ilivyo ni kwamba hawa wanachukuliwa wepesi. Matokeo yake mke anakaa faragha na kaka yake mume na hivyo ndio maana akafananishwa na kifo. Huyu ndiye ana haki zaidi ya kukatazwa.”[1]
ash-Shawkaaniy amesema katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Maneno yake “al-Hamuu ni kifo” bi maana kuwa na khofu juu yake ni kubwa kuliko kwa mwengine. Kama ambavyo khofu juu ya kifo ni kubwa zaidi kuliko juu ya kitu kingine.”[2]
Kwa hiyo basi, ee dada wa Kiislamu, mche Allaah na wala usichukulie wepesi jambo hili ikiwa wengine watafanya hivo. Kinachozingatiwa ni vile inavosema hukumu ya Kishari´ah na sio walivyozowea watu.
[1] (09/331).
[2] (06/122).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 124-125
- Imechapishwa: 11/12/2019
Hakika baadhi ya wanawake na wasimamizi wao wanachukulia wepesi kwa aina mbalimbali za ukaaji faragha ikiwa ni pamoja na:
a) Mwanamke kukaa faragha pamoja na ndugu zake mume pamoja na kuacha wazi uso wake mbele yao. Faragha hii ina khatari zaidi kuliko nyingine. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Tahadharini na kuingia sehemu za wanawake.” Mtu mmoja katika Answaar akasema: “Ee Mtume wa Allaah! Unasemaje kuhusu al-Hamuu.” Akajibu: “al-Hamuu ni kifo.”
Ameipokea Ahmad, al-Bukhaariy, at-Tirmidhiy na akaisahihisha.
Maana ya al-Hamuu ni yule ndugu yake mume. Kama kwamba alichukia kukaa naye faragha. al-Haafidhw bin Hajar amesema katika “Fath-ul-Baariy”:
“Wanachuoni wa lugha wameafikiana juu ya kwamba al-Ahmaa´ (mashemeji) ni wale ndugu zake mume wa mke; kama baba yake mume, kaka yake mume, mtoto wa kaka yake, mabinamu na mfano wao.” Akasema tena: “Makusudio katika Hadiyth ni wale ndugu zake mume – mbali na wale baba zake na watoto wake; kwa sababu hao ni Mahram zake mke na inafaa kwao kukaa naye faragha na hawaitwi kuwa ni kifo – kimazowea ilivyo ni kwamba hawa wanachukuliwa wepesi. Matokeo yake mke anakaa faragha na kaka yake mume na hivyo ndio maana akafananishwa na kifo. Huyu ndiye ana haki zaidi ya kukatazwa.”[1]
ash-Shawkaaniy amesema katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Maneno yake “al-Hamuu ni kifo” bi maana kuwa na khofu juu yake ni kubwa kuliko kwa mwengine. Kama ambavyo khofu juu ya kifo ni kubwa zaidi kuliko juu ya kitu kingine.”[2]
Kwa hiyo basi, ee dada wa Kiislamu, mche Allaah na wala usichukulie wepesi jambo hili ikiwa wengine watafanya hivo. Kinachozingatiwa ni vile inavosema hukumu ya Kishari´ah na sio walivyozowea watu.
[1] (09/331).
[2] (06/122).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 124-125
Imechapishwa: 11/12/2019
https://firqatunnajia.com/72-makatazo-ya-mke-kukaa-faragha-na-mashemeji/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)