Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته
“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume!”
Wamuombea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amani, rehema na baraka. Anaombewa, na wala haombwi pamoja na Allaah.
MAELEZO
Hii ni dalili juu ya kwamba hastahiki kuabudiwa. Wewe unamuombea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usalama, rehema na baraka. Kwa hiyo yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni mwenye kuhitaji. Mwenye kuhitaji hawi mungu wala mwabudiwa. Kuhusu Allaah hakuna yeyote amuombeaye usalama, rehema na baraka. Kwa sababu Yeye ndiye as-Salaam na amani inatoka Kwake. Yeye ndiye Mola wa wote na aliye juu yao. Hakuna yeyote aliye juu Yake mpaka aombewe. Hilo ni tofauti na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye ni kiumbe na ndiye mtu mtukufu zaidi. Allaah amemtukuza kwa unabii, ´ibaadah na ujumbe. Yeye ni mja na Mtume ambaye anatakiwa kutiiwa, kufuatwa, kusadikishwa na kupendwa zaidi ya inavopendwa pesa na nafsi. Lakini hata hivyo haabudiwi. ´Ibaadah ni haki ya Allaah. Yeyote anayemwabudu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi ameitekeleza haki ya Allaah kwenda kwa mwengine.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 97
- Imechapishwa: 28/06/2022
Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته
“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume!”
Wamuombea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amani, rehema na baraka. Anaombewa, na wala haombwi pamoja na Allaah.
MAELEZO
Hii ni dalili juu ya kwamba hastahiki kuabudiwa. Wewe unamuombea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usalama, rehema na baraka. Kwa hiyo yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni mwenye kuhitaji. Mwenye kuhitaji hawi mungu wala mwabudiwa. Kuhusu Allaah hakuna yeyote amuombeaye usalama, rehema na baraka. Kwa sababu Yeye ndiye as-Salaam na amani inatoka Kwake. Yeye ndiye Mola wa wote na aliye juu yao. Hakuna yeyote aliye juu Yake mpaka aombewe. Hilo ni tofauti na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye ni kiumbe na ndiye mtu mtukufu zaidi. Allaah amemtukuza kwa unabii, ´ibaadah na ujumbe. Yeye ni mja na Mtume ambaye anatakiwa kutiiwa, kufuatwa, kusadikishwa na kupendwa zaidi ya inavopendwa pesa na nafsi. Lakini hata hivyo haabudiwi. ´Ibaadah ni haki ya Allaah. Yeyote anayemwabudu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi ameitekeleza haki ya Allaah kwenda kwa mwengine.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 97
Imechapishwa: 28/06/2022
https://firqatunnajia.com/67-mtume-anaombewa-na-haombwi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)