Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema baina ya Sujuud mbili:
1-
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي وارْحَمْني وَاهدِني وَاجْبرْني وَعَافِنِي وَارْزُقْني
“Ee Allaah! Nisamehe, nihurumie, niongoze, niunge, niafu na uniruzuku.”[1]
Katika matamshi mengine imekuja:
رَبِّ اغْفِرْ لِي وارْحَمْني وَاهدِني وَاجْبرْني وَعَافِنِي وَارْزُقْني
“Ee Mola! Nisamehe, nihurumie, niongoze, niunge, niafu na uniruzuku.”
Mara nyingine akisema:
رَبِّ اغْفِرْ لِي ربِّ اغْفِرْ لي
“Ee Mola! Nisamehe! Ee Mola! Nisamehe!”[2]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akizisoma katika swalah ya usiku[3].
Halafu analeta Takbiyr na anasujudu Sujuud ya pili[4]. Alimwamrisha kufanya hivo yule mtu aliyeswali kimakosa na kumwambia baada ya kumwamrisha kutulia baina ya Sujuud mbili:
“Kisha useme:
الله اكبر
“Allaah ni mkubwa.”
Kisha sujudu mpaka kila mfupa utulie mahala pake. [Halafu ufanye hivo katika swalah yako yote iliyobaki.]”[5]
Wakati mwingine (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akinyanyua mikono sambamba na Takbiyr hii[6].
Akifanya katika Sujuud hii kama alivyofanya katika ile Sujuud ya kwanza. Halafu akinyanyua kichwa chake na kusema:
الله اكبر
“Allaah ni mkubwa.”
Alimwamrisha kufanya hivo yule mtu aliyeswali kimakosa[7] na kumwambia:
“Halafu ufanye hivo katika kila Rak´ah na kila Sajdah. Iwapo utafanya hivo, basi swalah yako imetimia, na ukipunguza kitu kwayo, kumepungua kutoka katika swalah yako.”[8]
Wakati mwingine alikuwa anaweza kunyanyua mikono yake[9].
[1] Abu Daawuud, at-Tirmidhiy, Ibn Maajah na al-Haakim ambaye ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
[2] Ibn Maajah kwa mlolongo wa wapokezi mzuri. Imaam Ahmad amechagua du´aa hii. Ishaaq bin Raahuuyah amesema:
“Ima aisome mara tatu au asome:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي وارْحَمْني وَاهدِني وَاجْبرْني وَعَافِنِي وَارْزُقْني
“Ee Allaah! Nisamehe, nihurumie, niongoze, niunge, niafu na uniruzuku.”
Kwa sababu zote mbili zimepokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baina ya Sujuud mbili.” (Masaa-il-ul-Imaam Ahmad wa Ishaaq bin Raahuuyah, uk. 19, ya Ishaaq al-Marwaziy)
[3] Haina maana kwamba haikuwekwa katika Shari´ah kusoma hivo katika swalah za faradhi kwa sababu hakuna tofauti kati ya swalah ya faradhi na ya Sunnah, kama alivyosema ash-Shaafi´iy, Ahmad na Ishaaq. Wanaonelea kuwa kitendo hicho kinafaa katika swalah ya faradhi na ya sunnah, kama alivyotaja at-Tirmidhiy. Hata at-Twahaawiy anaonelea kuwa kitendo hicho kimewekwa katika Shari´ah, kama ilivyotajwa katika kitabu “Mushkil-ul-Aathaar”. Kipimo sahihi kinatilia nguvu hili. Kwa sababu hakuna sehemu yoyote katika swalah ambayo haikuwekwa katika Shari´ah kusoma kitu. Kwa hivyo ni lazima hali iwe hivo sehemu hii. Ni jambo liko wazi.
[4] al-Bukhaariy na Muslim.
[5] Abu Daawuud na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Nyongeza imepokelewa na al-Bukhaariy na Muslim.
[6] Abu ´Awaanah na Abu Daawuud kwa isnadi mbili Swahiyh. Kunyanyua mikono huku ni maoni ya Ahmad na pia maoni ya Maalik na ash-Shaafi´iy.
[7] Abu Daawuud na al-Haakim ambaye ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
[8] Ahmad na at-Tirmidhiy aliyeisahihisha.
[9] Abu ´Awaanah na Abu Daawuud kwa isnadi mbili Swahiyh. Kunyanyua mikono huku ni maoni ya Ahmad na pia maoni ya Maalik na ash-Shaafi´iy.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 133-134
- Imechapishwa: 07/08/2017
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema baina ya Sujuud mbili:
1-
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي وارْحَمْني وَاهدِني وَاجْبرْني وَعَافِنِي وَارْزُقْني
“Ee Allaah! Nisamehe, nihurumie, niongoze, niunge, niafu na uniruzuku.”[1]
Katika matamshi mengine imekuja:
رَبِّ اغْفِرْ لِي وارْحَمْني وَاهدِني وَاجْبرْني وَعَافِنِي وَارْزُقْني
“Ee Mola! Nisamehe, nihurumie, niongoze, niunge, niafu na uniruzuku.”
Mara nyingine akisema:
رَبِّ اغْفِرْ لِي ربِّ اغْفِرْ لي
“Ee Mola! Nisamehe! Ee Mola! Nisamehe!”[2]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akizisoma katika swalah ya usiku[3].
Halafu analeta Takbiyr na anasujudu Sujuud ya pili[4]. Alimwamrisha kufanya hivo yule mtu aliyeswali kimakosa na kumwambia baada ya kumwamrisha kutulia baina ya Sujuud mbili:
“Kisha useme:
الله اكبر
“Allaah ni mkubwa.”
Kisha sujudu mpaka kila mfupa utulie mahala pake. [Halafu ufanye hivo katika swalah yako yote iliyobaki.]”[5]
Wakati mwingine (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akinyanyua mikono sambamba na Takbiyr hii[6].
Akifanya katika Sujuud hii kama alivyofanya katika ile Sujuud ya kwanza. Halafu akinyanyua kichwa chake na kusema:
الله اكبر
“Allaah ni mkubwa.”
Alimwamrisha kufanya hivo yule mtu aliyeswali kimakosa[7] na kumwambia:
“Halafu ufanye hivo katika kila Rak´ah na kila Sajdah. Iwapo utafanya hivo, basi swalah yako imetimia, na ukipunguza kitu kwayo, kumepungua kutoka katika swalah yako.”[8]
Wakati mwingine alikuwa anaweza kunyanyua mikono yake[9].
[1] Abu Daawuud, at-Tirmidhiy, Ibn Maajah na al-Haakim ambaye ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
[2] Ibn Maajah kwa mlolongo wa wapokezi mzuri. Imaam Ahmad amechagua du´aa hii. Ishaaq bin Raahuuyah amesema:
“Ima aisome mara tatu au asome:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي وارْحَمْني وَاهدِني وَاجْبرْني وَعَافِنِي وَارْزُقْني
“Ee Allaah! Nisamehe, nihurumie, niongoze, niunge, niafu na uniruzuku.”
Kwa sababu zote mbili zimepokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baina ya Sujuud mbili.” (Masaa-il-ul-Imaam Ahmad wa Ishaaq bin Raahuuyah, uk. 19, ya Ishaaq al-Marwaziy)
[3] Haina maana kwamba haikuwekwa katika Shari´ah kusoma hivo katika swalah za faradhi kwa sababu hakuna tofauti kati ya swalah ya faradhi na ya Sunnah, kama alivyosema ash-Shaafi´iy, Ahmad na Ishaaq. Wanaonelea kuwa kitendo hicho kinafaa katika swalah ya faradhi na ya sunnah, kama alivyotaja at-Tirmidhiy. Hata at-Twahaawiy anaonelea kuwa kitendo hicho kimewekwa katika Shari´ah, kama ilivyotajwa katika kitabu “Mushkil-ul-Aathaar”. Kipimo sahihi kinatilia nguvu hili. Kwa sababu hakuna sehemu yoyote katika swalah ambayo haikuwekwa katika Shari´ah kusoma kitu. Kwa hivyo ni lazima hali iwe hivo sehemu hii. Ni jambo liko wazi.
[4] al-Bukhaariy na Muslim.
[5] Abu Daawuud na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Nyongeza imepokelewa na al-Bukhaariy na Muslim.
[6] Abu ´Awaanah na Abu Daawuud kwa isnadi mbili Swahiyh. Kunyanyua mikono huku ni maoni ya Ahmad na pia maoni ya Maalik na ash-Shaafi´iy.
[7] Abu Daawuud na al-Haakim ambaye ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
[8] Ahmad na at-Tirmidhiy aliyeisahihisha.
[9] Abu ´Awaanah na Abu Daawuud kwa isnadi mbili Swahiyh. Kunyanyua mikono huku ni maoni ya Ahmad na pia maoni ya Maalik na ash-Shaafi´iy.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 133-134
Imechapishwa: 07/08/2017
https://firqatunnajia.com/65-adhkaar-kati-ya-sujuud-mbili/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)