Abu Muhammad ´Abdullaah bin Abiy Zayd al-Qayrawaaniy (Rahimahu Allaah) amesema:
Kutokana na ujuzi na makadirio Yake yaliyokwishatangulia kila mmoja amewepesishiwa juu ya kula maangamivu au furaha.
MAELEZO
Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Yale tunayofanya yamekwishapangwa au hayajapangwa?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Yamekwishapangwa.” Maswahabah wakasema: “Si tutegemee basi tuliyoandikiwa na tuache kutenda?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Fanyeni matendo! Kwani hakika kila mmoja ni mwenye kufanyiwa wepesi juu ya kile alichoumbiwa.” Kisha akasoma:
فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ
“Basi yule anayetoa na akamcha Allaah na akasadikisha lililo jema zaidi, basi tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi. Ama yule afanyaye ubakhili na akajiona amejitosheleza na akakadhibisha lililo jema zaidi, basi tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu.”[1]
Akabainisha (Subhaanah) kwamba uongofu na upotofu yanatokamana na mja, jambo ambalo ni uadilifu na fadhilah za Allaah.
[1] 92:5-10 al-Bukhaariy (4949) na Muslim (2647).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 48
- Imechapishwa: 05/08/2021
Abu Muhammad ´Abdullaah bin Abiy Zayd al-Qayrawaaniy (Rahimahu Allaah) amesema:
Kutokana na ujuzi na makadirio Yake yaliyokwishatangulia kila mmoja amewepesishiwa juu ya kula maangamivu au furaha.
MAELEZO
Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Yale tunayofanya yamekwishapangwa au hayajapangwa?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Yamekwishapangwa.” Maswahabah wakasema: “Si tutegemee basi tuliyoandikiwa na tuache kutenda?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Fanyeni matendo! Kwani hakika kila mmoja ni mwenye kufanyiwa wepesi juu ya kile alichoumbiwa.” Kisha akasoma:
فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ
“Basi yule anayetoa na akamcha Allaah na akasadikisha lililo jema zaidi, basi tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi. Ama yule afanyaye ubakhili na akajiona amejitosheleza na akakadhibisha lililo jema zaidi, basi tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu.”[1]
Akabainisha (Subhaanah) kwamba uongofu na upotofu yanatokamana na mja, jambo ambalo ni uadilifu na fadhilah za Allaah.
[1] 92:5-10 al-Bukhaariy (4949) na Muslim (2647).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 48
Imechapishwa: 05/08/2021
https://firqatunnajia.com/60-kila-kitu-kumewepesishwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)