6. Mnasemaje kuhusu maneno ya Allaah na Qur-aan?

Swali 6: Mnasemaje kuhusu maneno ya Allaah na Qur-aan?

Jibu: Qur-aan ni maneno ya Allaah, imeteremshwa na haikuumbwa. Imeanza Kwake na itarudi Kwake.

Allaah ndiye mwenye kutamka kwayo kikweli, matamshi yake na maana yake. Hakuacha na hatoacha kuwa mwenye kuzungumza siku zote kwa anayoyataka na pale anapotaka.

Maneno yake hayaishi na wala hayatoisha.

  • Mhusika: Imaam ´Abdur-Rahmaan bin Naaswir as-Sa´diy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahamm-ul-Muhimmaat, uk. 36
  • Imechapishwa: 25/03/2017