Qutbiyyuun Misri wanawapiga vita Salafiyyuun Misri na sehemu nyinginezo kwa njia ya ukundi [Hizbiyyah]. Wanawaita kuwa ni “wakosoaji wavuka mipaka” na wana mapenzi kwa Qutbiyyuun wengine, al-Ikhwaan al-Muslimuun, Abul-Hasan al-Miswriy al-Ma´ribiy na al-Halabiy na kundi lake.

Allaah Alifichua ujinasibishaji wao wa kimadai na Salafiyyah wakati mpetukaji mipaka Ikhwaaniy ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq alipotembelea Misri. Alimpokea kama mfalme na kusema kuwa ni Shaykh na kiongozi wao na kiongozi wa kiroho wa Salafiyyah, yaani Salafiyyah yao feki. Tovuti “Kull-us-Salafiyyiyn” ilituma masifa kwa ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq na watu wanaodai Salafiyyah. Kwenye tovuti kulikuwa yafuatayo:

“Ilikuwa ni muonekano mzuri kabisa na umati wa watu. Chaneli al-Hikmah al-Islaamiyyah ilikuja kwenye kiwanja kikuu cha ndege cha Cairo mahali pa kuwapokea wasafiri akiwa pamoja na Shaykh Abu Ishaaq al-Huwayniy na wamisri wengine wanaojulikana. Hapo ndipo aliposhuka baba wa kiroho wa Salafiyyah Shaykh ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq baada ya kutokuwepo kwa miaka thelathini…

Karibu na sehemu ya kutokea kwenye uwanja wa ndege kukapazwa Takbiyraat kwa wingi zilizosababisha mtetemeko… Marudio ya Salafiyyah Misri na katika ulimwengu wa Kiislamu ni kiongozi wa kiroho wa Salafiyyah. Tunampenda kwa ajili ya Allaah…”

al-Halabiy alijua kukaribishwa kwa ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq na kujifanya anakemea jambo hilo. Pamoja na hivyo anaonelea kuwa ni Salafiyyuun. Hatimae wakashirikiana na al-Ikhwaan juu ya mbiu yao ya kisekula na kusimamisha nchi ya kisekula na kidemokrasia isiyotofautisha kati ya waislamu na manaswara. Walishirikiana nao juu ya kuondosha hukumu ya Allaah katika vipengele vyote na wakasahau mbiu yao ya zamani ya kwamba Allaah Pekee ndiye mwenye haki ya kuhukumu. Baadhi yao walikuwa wakimfanyia Takfiyr ya wazi yule asiyehukumu kwa hukumu ya Allaah pasina kupata upingamizi wowote.

Je, ushuhudiaji wa al-Halabiy ya kwamba wao ni Salafiyyuun si ni mfano wa uongo ulio mkubwa, mgongano mkubwa na ushuhudiaji mkubwa wa uongo?

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://rabee.net/ar/articles.php?cat=8&id=236
  • Imechapishwa: 08/01/2017