Ee mwanamke wa Kiislamu! Ni lazima kwako kumtii mume wako kwa wema. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ataposwali mwanamke vipindi vyake vitano, akahifadhi tupu yake na akamtii mume wake, basi ataingia kupitia mlango wowote wa Peponi anaotaka.”
Ameipokea Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh” yake.
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Si halali kwa mwanamke kufunga na mume wake yuko isipokuwa kwa idhini yake.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mume atapomwita mke wake kitandani na asije akalala na huku amemkasirikia, basi hulaaniwa na Malaika mpaka kupambazuke.”
Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim na wengineo.
Katika upokezi wa al-Bukhaariy na Muslim Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ninaapa kwa ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake. Hakuna mwanamume ambaye anamwita mke wake kitandani ambapo akamkatalia isipokuwa Ambaye yuko juu ya mbingu humkasirikia.”
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 106-107
- Imechapishwa: 20/11/2019
Ee mwanamke wa Kiislamu! Ni lazima kwako kumtii mume wako kwa wema. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ataposwali mwanamke vipindi vyake vitano, akahifadhi tupu yake na akamtii mume wake, basi ataingia kupitia mlango wowote wa Peponi anaotaka.”
Ameipokea Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh” yake.
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Si halali kwa mwanamke kufunga na mume wake yuko isipokuwa kwa idhini yake.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mume atapomwita mke wake kitandani na asije akalala na huku amemkasirikia, basi hulaaniwa na Malaika mpaka kupambazuke.”
Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim na wengineo.
Katika upokezi wa al-Bukhaariy na Muslim Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ninaapa kwa ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake. Hakuna mwanamume ambaye anamwita mke wake kitandani ambapo akamkatalia isipokuwa Ambaye yuko juu ya mbingu humkasirikia.”
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 106-107
Imechapishwa: 20/11/2019
https://firqatunnajia.com/58-mwanamke-kumtii-mume-wake-na-kutomuasi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)