Imependekezwa kwa wanawake kupiga dufu ili ndoa itangazike na ienee na hayo yanafanyika kati ya wanawake peke yao. Dufu hilo lisiambatane na muziki, ala za pumbao wala sauti nzuri za wanawake. Katika mnasaba huu hakuna neno kwa wanawake kuimba mashairi kwa njia ya kwamba wasisikiwe na wanaume. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kipambanuzi kati ya halali na haramu ni dufu na sauti katika ndoa.”
Imaam ash-Shawkaaniy amesema katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Katika hayo kuna dalili inayoonyesha kuwa inafaa kwa wanawake kupiga dufu na kunyanyua sauti zao kwa kitu katika maneno kama mfano wa:
أتيناكم أتيناكم
“Tumekujieni, tumekujieni… “
na mfano wake. Si kwa nyimbo zenye kuamsha maovu, kusifu uzuri, madhambi na kunywa kwa pombe. Hayo ni haramu ndani ya ndoa kama ilivyo pia haramu kwenginepo. Vivyo hivyo pumbazo zengine zote zilizoharamu.”
Ee dada wa Kiislamu! Usifanye israfu katika kununua vitu vya kujipamba na nguo katika mnasaba wa ndoa. Matendo haya ni israfu ambayo imekatazwa na Allaah na akaeleza kwamba hawapendi wenye kufanya hivo. Amesema (Ta´ala):
وَلَا تُسْرِفُوا ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُسْرِفِينَ
“Wala msifanye israfu. Hakika Yeye hawapendi wafanyao israfu.”[1]
Fanya mambo kati na kati na achana na mambo ya kujifakharisha.
[1] 06:141
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 106
- Imechapishwa: 20/11/2019
Imependekezwa kwa wanawake kupiga dufu ili ndoa itangazike na ienee na hayo yanafanyika kati ya wanawake peke yao. Dufu hilo lisiambatane na muziki, ala za pumbao wala sauti nzuri za wanawake. Katika mnasaba huu hakuna neno kwa wanawake kuimba mashairi kwa njia ya kwamba wasisikiwe na wanaume. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kipambanuzi kati ya halali na haramu ni dufu na sauti katika ndoa.”
Imaam ash-Shawkaaniy amesema katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Katika hayo kuna dalili inayoonyesha kuwa inafaa kwa wanawake kupiga dufu na kunyanyua sauti zao kwa kitu katika maneno kama mfano wa:
أتيناكم أتيناكم
“Tumekujieni, tumekujieni… “
na mfano wake. Si kwa nyimbo zenye kuamsha maovu, kusifu uzuri, madhambi na kunywa kwa pombe. Hayo ni haramu ndani ya ndoa kama ilivyo pia haramu kwenginepo. Vivyo hivyo pumbazo zengine zote zilizoharamu.”
Ee dada wa Kiislamu! Usifanye israfu katika kununua vitu vya kujipamba na nguo katika mnasaba wa ndoa. Matendo haya ni israfu ambayo imekatazwa na Allaah na akaeleza kwamba hawapendi wenye kufanya hivo. Amesema (Ta´ala):
وَلَا تُسْرِفُوا ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُسْرِفِينَ
“Wala msifanye israfu. Hakika Yeye hawapendi wafanyao israfu.”[1]
Fanya mambo kati na kati na achana na mambo ya kujifakharisha.
[1] 06:141
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 106
Imechapishwa: 20/11/2019
https://firqatunnajia.com/57-hukumu-ya-wanawake-kupiga-dufu-kwa-ajili-ya-kutangaza-ndoa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)