Imaam Ibn Abiy Daawuud (Rahimahu Allaah) amesema:
ومن بعدهم فالتابعون لحسن مآخذ
24 – Walioko baada yao ni Taabi´uun kwa uchukuliaji wao mzuri
وأفعالهم قولا وفعلا فأفلحوا
ni sawa katika matendo na maneno yao na hivyo wakawa ni wenye kufaulu
ومالك والثوري ثم أخوهم
25 – Pia na Maalik, ath-Thawriy na halafu ndugu zao
أبو عمرو الأوزاعي ذاك المسبح
Abu ´Amr al-Awzaa´iy ambaye ni mwenye kusifiwa
ومن بعدهم فالشافعي وأحمد
26 – Waliokuja baada yao ambaye ni ash-Shaafi´iy na Ahmad
إماما هدى من يتبع الحق ينصح
ni imamu wa uongofu mwenye kufuata haki na kunasihi
أولــئك قوم قـد عفا الله عنهم
27 – Hao ni watu waliosamehewa na Allaah
فاحببهـم فإنـك تــفرح
hivyo basi wapende, hakika utafurahi
MAELEZO
Wanaofuatia baada ya Maswahabah ni Taabi´uun. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ
“Na wale waliotangulia awali katika Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema.” (09:100)
Maneno Yake:
وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ
“… na wale waliowafuata kwa wema.”
yanajumuisha wale wote waliowafuata kwa wema hadi siku ya Qiyaamah. Lakini kunaposewa neno “Taabi´iy” kunakusudiwa yule ambaye alichukua elimu na akasoma kutoka kwa Swahabah. Vinginevyo neno “mfuataji” linamkusanya kila yule ambaye alichukua na kufuata mfumo wa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuanzia wale wa mwanzo, ambao walikuwa baada ya Maswahabah na wa mwisho. Kwa ajili hii amesema (Jalla wa ´Alaa) baada ya kuwataja Muhaajiruun na Answaar:
وَالَّذِينَ جَاءُوا مِن بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ
“Na wale waliokuja baada yao wanasema: “Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa imani na wala Usijaalie katika nyoyo zetu mafundo ya chuki kwa wale walioamini. Mola wetu! Hakika Wewe ni Mwenye huruma, Mwenye kurehemu.” (59:10)
Katika Aayah hii kuna Radd kwa Raafidhwah ambao wanawachukia Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa mioyo yao na wanatamka kwa ndimi zao. Bali wanawalaani kabisa na kuwakufurisha Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa ajili hii ndio maana Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
“Miongoni mwa misingi ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kuwa na mioyo na ndimi safi kwa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]
Wana mioyo safi kutokana na maneno Yake:
وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا
“… na wala Usijaalie katika nyoyo zetu mafundo ya chuki.”
Vilevile wana ndimi safi kutokana na maneno Yake:
يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ
“Wanasema: “Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa imani.””
Katika Aayah hii kuna mafunzo ya kwamba inatakiwa kwa mtu awe na moyo na ulimi mzuri kwa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Huu ndio mfumo wa wale wenye kuwafuata kwa wema.
Kuhusu wale ambao wanajeruhi, kupekua kasoro, kueneza shaka juu ya fadhilah za Maswahabah, kuwakufurisha na kuwalaani, haya ni mambo yanayoenda kinyume na mfumo wa Kiislamu, anaufanyia uadui Uislamu na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa sababu akiwatukana Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ina maana amemtukana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Vilevile ameitukana Qur-aan inayowasifu.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Pia na Maalik, ath-Thawriy na halafu ndugu… “
Mtunzi (Rahimahu Allaah) anataja fadhilah za maimamu. Miongoni mwao ni maimamu hawa:
Maalik mkusudiwa ni Maalik bin Anas ambaye ni Imaam wa al-Madiynah.
ath-Thawriy mkusudiwa ni Sufyaan ath-Thawriy.
al-Awzaa´iy mkusudiwa ni Imaam wa watu wa Shaam.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Waliokuja baada yao ambaye ash-Shaafi´iy na Ahmad.”
Ni Muhammad bin Idriys ash-Shaafi´iy na Ahmad bin Hanbal.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Hivyo basi wapende hakika utafurahi.”
Wapende as-Salaf as-Swaalih na maimamu wa Uislamu. Hakika kufanya hivo ni alama ya imani.
Hakumtaja Abu Haniyfah kwa kuwa imesemekana kuwa yeye ni katika Taabi´uun na kwamba alikutana na kundi la Maswahabah. Maoni sahihi ni kwamba yeye ni katika waliokuja baada ya Taabi´uun. Hakukutana na Maswahabah. Alikutana na Taabi´uun. Yeye ni mtu wa karne ya tatu ambayo ni moja ya zile karne bora (Rahimahu Allaah). Yeye ndiye imamu wa kwanza miongoni mwa wale maimamu wanne inapokuja katika zama.
[1] ´Aqiydah al-Waasitwiyyah katika “Majmuu´-ul-Fataawaa” (03/152).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 130-132
- Imechapishwa: 11/01/2024
Imaam Ibn Abiy Daawuud (Rahimahu Allaah) amesema:
ومن بعدهم فالتابعون لحسن مآخذ
24 – Walioko baada yao ni Taabi´uun kwa uchukuliaji wao mzuri
وأفعالهم قولا وفعلا فأفلحوا
ni sawa katika matendo na maneno yao na hivyo wakawa ni wenye kufaulu
ومالك والثوري ثم أخوهم
25 – Pia na Maalik, ath-Thawriy na halafu ndugu zao
أبو عمرو الأوزاعي ذاك المسبح
Abu ´Amr al-Awzaa´iy ambaye ni mwenye kusifiwa
ومن بعدهم فالشافعي وأحمد
26 – Waliokuja baada yao ambaye ni ash-Shaafi´iy na Ahmad
إماما هدى من يتبع الحق ينصح
ni imamu wa uongofu mwenye kufuata haki na kunasihi
أولــئك قوم قـد عفا الله عنهم
27 – Hao ni watu waliosamehewa na Allaah
فاحببهـم فإنـك تــفرح
hivyo basi wapende, hakika utafurahi
MAELEZO
Wanaofuatia baada ya Maswahabah ni Taabi´uun. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ
“Na wale waliotangulia awali katika Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema.” (09:100)
Maneno Yake:
وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ
“… na wale waliowafuata kwa wema.”
yanajumuisha wale wote waliowafuata kwa wema hadi siku ya Qiyaamah. Lakini kunaposewa neno “Taabi´iy” kunakusudiwa yule ambaye alichukua elimu na akasoma kutoka kwa Swahabah. Vinginevyo neno “mfuataji” linamkusanya kila yule ambaye alichukua na kufuata mfumo wa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuanzia wale wa mwanzo, ambao walikuwa baada ya Maswahabah na wa mwisho. Kwa ajili hii amesema (Jalla wa ´Alaa) baada ya kuwataja Muhaajiruun na Answaar:
وَالَّذِينَ جَاءُوا مِن بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ
“Na wale waliokuja baada yao wanasema: “Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa imani na wala Usijaalie katika nyoyo zetu mafundo ya chuki kwa wale walioamini. Mola wetu! Hakika Wewe ni Mwenye huruma, Mwenye kurehemu.” (59:10)
Katika Aayah hii kuna Radd kwa Raafidhwah ambao wanawachukia Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa mioyo yao na wanatamka kwa ndimi zao. Bali wanawalaani kabisa na kuwakufurisha Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa ajili hii ndio maana Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
“Miongoni mwa misingi ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kuwa na mioyo na ndimi safi kwa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]
Wana mioyo safi kutokana na maneno Yake:
وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا
“… na wala Usijaalie katika nyoyo zetu mafundo ya chuki.”
Vilevile wana ndimi safi kutokana na maneno Yake:
يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ
“Wanasema: “Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa imani.””
Katika Aayah hii kuna mafunzo ya kwamba inatakiwa kwa mtu awe na moyo na ulimi mzuri kwa Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Huu ndio mfumo wa wale wenye kuwafuata kwa wema.
Kuhusu wale ambao wanajeruhi, kupekua kasoro, kueneza shaka juu ya fadhilah za Maswahabah, kuwakufurisha na kuwalaani, haya ni mambo yanayoenda kinyume na mfumo wa Kiislamu, anaufanyia uadui Uislamu na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa sababu akiwatukana Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ina maana amemtukana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Vilevile ameitukana Qur-aan inayowasifu.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Pia na Maalik, ath-Thawriy na halafu ndugu… ”
Mtunzi (Rahimahu Allaah) anataja fadhilah za maimamu. Miongoni mwao ni maimamu hawa:
Maalik mkusudiwa ni Maalik bin Anas ambaye ni Imaam wa al-Madiynah.
ath-Thawriy mkusudiwa ni Sufyaan ath-Thawriy.
al-Awzaa´iy mkusudiwa ni Imaam wa watu wa Shaam.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Waliokuja baada yao ambaye ash-Shaafi´iy na Ahmad.”
Ni Muhammad bin Idriys ash-Shaafi´iy na Ahmad bin Hanbal.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Hivyo basi wapende hakika utafurahi.”
Wapende as-Salaf as-Swaalih na maimamu wa Uislamu. Hakika kufanya hivo ni alama ya imani.
Hakumtaja Abu Haniyfah kwa kuwa imesemekana kuwa yeye ni katika Taabi´uun na kwamba alikutana na kundi la Maswahabah. Maoni sahihi ni kwamba yeye ni katika waliokuja baada ya Taabi´uun. Hakukutana na Maswahabah. Alikutana na Taabi´uun. Yeye ni mtu wa karne ya tatu ambayo ni moja ya zile karne bora (Rahimahu Allaah). Yeye ndiye imamu wa kwanza miongoni mwa wale maimamu wanne inapokuja katika zama.
[1] ´Aqiydah al-Waasitwiyyah katika “Majmuu´-ul-Fataawaa” (03/152).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 130-132
Imechapishwa: 11/01/2024
https://firqatunnajia.com/56-fadhila-za-baadhi-ya-maimamu-wa-ahl-us-sunnah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)