50. al-Qummiy upotoshaji wa kumi na moja wa al-Baqarah

al-Qummiy amesema:

“Kuhusiana na Aayah al-Kursiy, baba yangu amenihadithia, kutoka kwa al-Husayn bin Khaalid ya kwamba Abul-Hasan ar-Ridhwaa ameisoma namna hii:

الم اللّهُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ لاَ تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلاَ نَوْمٌ لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَمَا تَحْتَ الثَّرَى عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ هُوَ الرَّحْمَنُ الرَّحِيمُ

“Alif Laam Miym. Allaah – hapana mungu wa haki isipokuwa Yeye, Aliye hai na Mwenye kuyasimamia mambo. Haumchukuwi usingizi wala kulala[1]. Ni Vyake pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi na vilivyomo baina yao na vilivyomo chini ya ardhi[2]. Ni mjuzi wa vilivyofichikana na vyenye kuonekana – hakika Yeye ndiye Mwingi wa huruma, Mwenye kurehemu[3].”[4]

Mosi amezidisha (الم) Aliy Laam Miym mwanzoni mwa Aayah tukufu.

Pili ameongeza:

وَمَا بَيْنَهُمَا وَمَا تَحْتَ الثَّرَى عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ هُوَ الرَّحْمَنُ الرَّحِيمُ

“… na vilivyomo baina yao na vilivyomo chini ya ardhi. Ni mjuzi wa vilivyofichikana na vyenye kuonekana – hakika Yeye ndiye Mwingi wa huruma, Mwenye kurehemu.”

Ni yapi malengo ya nyongeza hii? Ndio, ni uzandiki na ujasiri kwa Allaah, Kitabu Chake na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Unaona namna ambavyo wanaipotosha Qur-aan kwa kiwango ambacho hata mayahudi na manaswara hawawezi. Halafu wanawatuhumu Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakweli na waaminifu ya kwamba wameongeza na kupunguza katika Qur-aan. Tuhuma hizi dhidi ya Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na (Radhiya Allaahu ´anhum) si jengine isipokuwa ni uongo na uzushi wa Raafidhwah na Baatwiniyyah.

[1] 02:255

[2] 20:06

[3] 59:22

[4] Tafsiyr al-Qummiy. (01/184).

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 82-83
  • Imechapishwa: 03/04/2017