5. al-Halabiy na taasisi ya Ihyaa´ at-Turaath

´Aliy al-Halabiy ni katika watu wabaya zaidi wanaoshuhudia batili. Anashuhudia kwa watu wapotevu na wenye misingi ilioharibika na mifumo batili ya kwamba ni Salafiyyuuun, amesimama upande wao na kutumia misingi na mifumo yao. Miongoni mwa watu hawa ni:

1- Taasisi ya kikuwait Ihyaa´ at-Turaath

Inafanya bidii kuwatenganisha na kuwatawanya Salafiyyuun ulimwenguni mzima. Wanaunda na kuajiri vyama ili kupiga vita mfumo wa Salaf. Mfano wa vyama hivyo ni al-Hikmah Yemen na ar-Rashad Indonesia iliyoundwa na watu wasiotofautisha kati ya Raafidhwah, Khawaarij na Ahl-us-Sunnah. Wana harakati vilevile India na Pakistan ili kuwatenganisha Salafiyyuun. Wana taathira mbaya sana katika nchi hizo.

Pamoja na yote hayo al-Halabiy na kundi lake wanashuhudia kwamba taasisi hii ni Salafiy pamoja na kuwa wanajua yale wanayoyafanya. Je, ushuhudiaji huu si mfano wa ushuhudiaji wa batili ilio kubwa na mgongano mkubwa wa mfumo wa Salaf?

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://rabee.net/ar/articles.php?cat=8&id=236
  • Imechapishwa: 08/01/2017