Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitulizana katika Rukuu´ na akamwamrisha hivo yule mtu aliyeswali kimakosa, kama tulivyotangulia kutaja.
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Timizeni Rukuu´ na Sujuud zenu. Ninaapa kwa Yule ambaye nafsi yangu iko mkononi Mwake ya kwamba mimi naweza kukuoneni nyuma yangu[1] pindi mnaporukuu na mnaposujudu.”[2]
Alimuona (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwanamume mmoja haitimizi Rukuu´ yake na anadonoa katika Sujuud yake akasema:
“Lau mtu huyu angelikufa katika hali hii basi angelikuwa amekufa katika dini isiyokuwa ya Muhammad. Anadonoa swalah yake kama adonoavyo kunguru damu. Mfano wa ambaye haitimizi Rukuu´ yake na anadonoa katika Sujuud yake ni kama mfano wa mtu ambaye anakula tende moja au mbili; hazimnufaishi kwa chochote.”[3]
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kipenzi wangu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amenikataza kuidonoa swalah yangu kama jogoo, kugeukageuka kama mbweha na kuchuchumaa kama ngedere.”[4]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwizi mbaya kabisa ni yule anayeiba katika swalah yake.” Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Ni vipi ataiba katika swalah yake?” Wakasema: “Hatimizi Rukuu´ wala Sujuud yake.”[5]
Wakati mmoja alipokuwa akiswali mara akamtupia jicho kupitia kwenye pembe ya jicho lake mtu ambaye alikuwa hanyooshi uti wa mgongo wake katika Rukuu´ na Sujuud. Alipomaliza akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Enyi waislamu! Haisihi swalah ya yule ambaye hasawazishi uti wa mgongo wake katika Rukuu´ na Sujuud.”[6]
Amesema katika Hadiyth nyingine:
“Swalah ya mtu haisihi mpaka asawazishe uti wa mgongo wake katika Rukuu´ na Sujuud.”[7]
[1] Kuona huku ni kwa hakika na ni moja katika miujiza yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hata hivyo ni jambo linahusiana katika swalah peke yake. Hakuna dalili ya kuona kwa ujumla.
[2] al-Bukhaariy na Muslim.
[3] Abu Ya´laa katika ”al-Musnad” (1/349), al-Aajurriy katika ”al-Arba´iyn”, al-Bayhaqiy , at-Twabaraaniy (1/192/1), adh-Dhwiyaa’ katika ”al-Muntaqaa” (1/276) na Ibn ´Asaakir (2/226/2) kwa mlolongo wa wapokezi mzuri. Imesahihishwa na Ibn Khuzaymah (1/82/1). Sehemu ya kwanza ya sentesi ina upokezi wenye kuutilia nguvu katika ”al-Ibaanah” (1/43/5) ya Ibn Battwah hata hivyo ni usimulizi ambao ni Mursal.
[4] at-Twayaalisiy, Ahmad na Ibn Abiy Shaybah. Hadiyth ni nzuri, kama nilivyoieleza katika taaliki zangu ya ”al-Ahkaam” (1348) ya Haafidhw ´Abdul-Haqq al-Ishbiyliy.
[5] Ibn Abiy Shaybah (2/89/1), at-Twabaraaniy na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
[6] Ibn Abiy Shaybah (1/89/1), Ibn Maajah na Ahmad kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh. Tazama ”as-Swahiyhah” (2536).
[7] Abu ´Awaanah, Abu Daawuud na as-Sahmiy (61). ad-Daaraqutwniy ameisahihisha.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 113-114
- Imechapishwa: 17/02/2017
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitulizana katika Rukuu´ na akamwamrisha hivo yule mtu aliyeswali kimakosa, kama tulivyotangulia kutaja.
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Timizeni Rukuu´ na Sujuud zenu. Ninaapa kwa Yule ambaye nafsi yangu iko mkononi Mwake ya kwamba mimi naweza kukuoneni nyuma yangu[1] pindi mnaporukuu na mnaposujudu.”[2]
Alimuona (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwanamume mmoja haitimizi Rukuu´ yake na anadonoa katika Sujuud yake akasema:
“Lau mtu huyu angelikufa katika hali hii basi angelikuwa amekufa katika dini isiyokuwa ya Muhammad. Anadonoa swalah yake kama adonoavyo kunguru damu. Mfano wa ambaye haitimizi Rukuu´ yake na anadonoa katika Sujuud yake ni kama mfano wa mtu ambaye anakula tende moja au mbili; hazimnufaishi kwa chochote.”[3]
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kipenzi wangu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amenikataza kuidonoa swalah yangu kama jogoo, kugeukageuka kama mbweha na kuchuchumaa kama ngedere.”[4]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwizi mbaya kabisa ni yule anayeiba katika swalah yake.” Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Ni vipi ataiba katika swalah yake?” Wakasema: “Hatimizi Rukuu´ wala Sujuud yake.”[5]
Wakati mmoja alipokuwa akiswali mara akamtupia jicho kupitia kwenye pembe ya jicho lake mtu ambaye alikuwa hanyooshi uti wa mgongo wake katika Rukuu´ na Sujuud. Alipomaliza akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Enyi waislamu! Haisihi swalah ya yule ambaye hasawazishi uti wa mgongo wake katika Rukuu´ na Sujuud.”[6]
Amesema katika Hadiyth nyingine:
“Swalah ya mtu haisihi mpaka asawazishe uti wa mgongo wake katika Rukuu´ na Sujuud.”[7]
[1] Kuona huku ni kwa hakika na ni moja katika miujiza yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hata hivyo ni jambo linahusiana katika swalah peke yake. Hakuna dalili ya kuona kwa ujumla.
[2] al-Bukhaariy na Muslim.
[3] Abu Ya´laa katika ”al-Musnad” (1/349), al-Aajurriy katika ”al-Arba´iyn”, al-Bayhaqiy , at-Twabaraaniy (1/192/1), adh-Dhwiyaa’ katika ”al-Muntaqaa” (1/276) na Ibn ´Asaakir (2/226/2) kwa mlolongo wa wapokezi mzuri. Imesahihishwa na Ibn Khuzaymah (1/82/1). Sehemu ya kwanza ya sentesi ina upokezi wenye kuutilia nguvu katika ”al-Ibaanah” (1/43/5) ya Ibn Battwah hata hivyo ni usimulizi ambao ni Mursal.
[4] at-Twayaalisiy, Ahmad na Ibn Abiy Shaybah. Hadiyth ni nzuri, kama nilivyoieleza katika taaliki zangu ya ”al-Ahkaam” (1348) ya Haafidhw ´Abdul-Haqq al-Ishbiyliy.
[5] Ibn Abiy Shaybah (2/89/1), at-Twabaraaniy na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.
[6] Ibn Abiy Shaybah (1/89/1), Ibn Maajah na Ahmad kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh. Tazama ”as-Swahiyhah” (2536).
[7] Abu ´Awaanah, Abu Daawuud na as-Sahmiy (61). ad-Daaraqutwniy ameisahihisha.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 113-114
Imechapishwa: 17/02/2017
https://firqatunnajia.com/48-uwajibu-wa-kutulizana-katika-rukuu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)