Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiweka vitanga vyake vya mikono juu ya magoti yake[1] na akawaamrisha Maswahabah kufanya vivyo hivyo[2]. Alimwamrisha vilevile yule mtu aliyeswali vibaya kufanya hivo kama tulivyotangulia kutaja punde.
Alikuwa akimakinisha mikono yake juu ya magoti yake kama vile ameyashikilia[3].
Alikuwa akitenganisha kati ya vidole vyake[4]. Alimwamrisha hivo yule mtu mwenye kuswali makosa na kusema:
“Unaporukuu basi viweke vitanga vya mikono yako juu ya magoti yako, tenganisha kati ya vidole vyako kisha ubaki hivyo mpaka kila kiungo cha mwili kitue pahali pake.”[5]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akijitawanya na akitenganisha visugudi vyake na mbavu zake[6].
Wakati anapoenda katika Rukuu´ anautandaza na kuuweka sawa mgongo wake[7]. Kiasi cha kwamba iwapo mtu angelimwaga maji juu ya mgongo wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yangelitulia[8]. Alimwambia mtu yule aliyeswali kimakosa:
“Unapoenda katika Rukuu´ basi weka vitanga vyako vya mikono juu ya magoti yako, unyooshe mgongo wako na tulizana kwenye Rukuu´ yako.”[9]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakiinamishi kichwa chake na wala hakiinui[10] isipokuwa kilikuwa baina yake.
[1] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
[2] al-Bukhaariy na Muslim.
[3] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
[4] at-Twayaalisiy na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Imetajwa katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (809).
[5] Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan katika ”as-Swahiyh” zao.
[6] at-Tirmidhiy aliyeisahihisha na Ibn Khuzaymah.
[7] al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh na al-Bukhaariy.
[8] at-Twabaraaniy katika ”al-Mu´jam al-Kabiyr” na ”al-Mu´jam as-Swaghiyr”, ´Abdullaah bin Ahmad katika ”Zawaa-id-ul-Musnad” na Ibn Maajah.
[9] Ahmad na Abu Daawuud kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[10] Abu Daawuud na al-Bukhaariy katika ”Juz-ul-Qiraa-ah” kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh. Maana ya hakiinui kichwa chake ina maana kwamba hakinyanyui zaidi ya kichwa chake mpaka kikawa juu zaidi ya mongo. Tazama ”an-Nihaayah”
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 112-113
- Imechapishwa: 17/02/2017
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiweka vitanga vyake vya mikono juu ya magoti yake[1] na akawaamrisha Maswahabah kufanya vivyo hivyo[2]. Alimwamrisha vilevile yule mtu aliyeswali vibaya kufanya hivo kama tulivyotangulia kutaja punde.
Alikuwa akimakinisha mikono yake juu ya magoti yake kama vile ameyashikilia[3].
Alikuwa akitenganisha kati ya vidole vyake[4]. Alimwamrisha hivo yule mtu mwenye kuswali makosa na kusema:
“Unaporukuu basi viweke vitanga vya mikono yako juu ya magoti yako, tenganisha kati ya vidole vyako kisha ubaki hivyo mpaka kila kiungo cha mwili kitue pahali pake.”[5]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akijitawanya na akitenganisha visugudi vyake na mbavu zake[6].
Wakati anapoenda katika Rukuu´ anautandaza na kuuweka sawa mgongo wake[7]. Kiasi cha kwamba iwapo mtu angelimwaga maji juu ya mgongo wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yangelitulia[8]. Alimwambia mtu yule aliyeswali kimakosa:
“Unapoenda katika Rukuu´ basi weka vitanga vyako vya mikono juu ya magoti yako, unyooshe mgongo wako na tulizana kwenye Rukuu´ yako.”[9]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakiinamishi kichwa chake na wala hakiinui[10] isipokuwa kilikuwa baina yake.
[1] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
[2] al-Bukhaariy na Muslim.
[3] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
[4] at-Twayaalisiy na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Imetajwa katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (809).
[5] Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan katika ”as-Swahiyh” zao.
[6] at-Tirmidhiy aliyeisahihisha na Ibn Khuzaymah.
[7] al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh na al-Bukhaariy.
[8] at-Twabaraaniy katika ”al-Mu´jam al-Kabiyr” na ”al-Mu´jam as-Swaghiyr”, ´Abdullaah bin Ahmad katika ”Zawaa-id-ul-Musnad” na Ibn Maajah.
[9] Ahmad na Abu Daawuud kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[10] Abu Daawuud na al-Bukhaariy katika ”Juz-ul-Qiraa-ah” kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh. Maana ya hakiinui kichwa chake ina maana kwamba hakinyanyui zaidi ya kichwa chake mpaka kikawa juu zaidi ya mongo. Tazama ”an-Nihaayah”
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 112-113
Imechapishwa: 17/02/2017
https://firqatunnajia.com/47-sifa-ya-rukuu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)