Miongoni mwa hekima ya funga ni kwamba ni sababu ya kumcha Allaah. Amesema (Subhaanahu wa Ta´ala):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
“Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa kufunga kama ilivyofaradhishwa kwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah.”[1]
Mfungaji ameamrishwa kufanya matendo mema na kujiepusha na matendo maovu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule asiyeacha maneno ya uongo, kuyatendea kazi na ujinga, basi Allaah hana haja kwa yeye kuacha chakula na kinywaji chake.”
Ameipokea al-Bukhaariy.
Ikiwa mfungaji ni mwenye kubabaika wakati wa funga basi kila ambapo atatamani kufanya maasi basi anakumbuka kuwa amefunga na hivyo anajizuia nayo. Kwa ajili hiyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemwamrisha mfungaji kumjibu yule mwenye kumtukana:
“Hakika mimi nimefunga.”
Huko ni kumzindua juu ya kwamba mfungaji ameamrishwa kujizuia kutukanana. Pia anaikumbusha nafsi yake kuwa amefunga na hivyo akajizuia kumkabili kwa matusi.
[1] 02:183
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 64
- Imechapishwa: 14/05/2020
Miongoni mwa hekima ya funga ni kwamba ni sababu ya kumcha Allaah. Amesema (Subhaanahu wa Ta´ala):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
“Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa kufunga kama ilivyofaradhishwa kwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah.”[1]
Mfungaji ameamrishwa kufanya matendo mema na kujiepusha na matendo maovu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule asiyeacha maneno ya uongo, kuyatendea kazi na ujinga, basi Allaah hana haja kwa yeye kuacha chakula na kinywaji chake.”
Ameipokea al-Bukhaariy.
Ikiwa mfungaji ni mwenye kubabaika wakati wa funga basi kila ambapo atatamani kufanya maasi basi anakumbuka kuwa amefunga na hivyo anajizuia nayo. Kwa ajili hiyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemwamrisha mfungaji kumjibu yule mwenye kumtukana:
“Hakika mimi nimefunga.”
Huko ni kumzindua juu ya kwamba mfungaji ameamrishwa kujizuia kutukanana. Pia anaikumbusha nafsi yake kuwa amefunga na hivyo akajizuia kumkabili kwa matusi.
[1] 02:183
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 64
Imechapishwa: 14/05/2020
https://firqatunnajia.com/46-hekima-ya-pili-ya-swawm-kumcha-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)