42. Akafiri vipi kwa kufanya jimaa miaka miwili iliyopita mchana wa Ramadhaan?

Swali 42: Miaka sita iliyopita kuna mtu alimjamii mke wake mchana wa Ramadhaan. Mpaka sasa hajatoa kafara. Ni lipi la wajibu kwake?

Jibu: Inategemea na hali yake. Haijuzu kwake kuchelewesha kafara. Ni wajibu kwake kutoa kafara. Ikiwa hawezi kufunga miezi miwili mfululizo, atoe kafara kwa kuwalisha masikini. Ikiwa anaweza kufunga basi ni lazima atoe kafara kwa kufunga.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaas-Swiyaam, uk. 61
  • Imechapishwa: 13/06/2017