Swali 29: Mimi ni mwanamke ambaye mimba yangu imeporomoka ndani ya mwezi wa tatu mwaka mmoja uliopita na sikuswali mpaka niliposafika. Nimeambiwa kwamba nilipaswa kuswali. Nifanye nini na mimi sijui idadi halisi ya siku?
Jibu: Kinachofahamika kwa wanachuoni ni kwamba mwanamke akiporomosha mimba ya miezi mitatu haswali. Kwa sababu mwanamke akiporomosha kipomoko ambaye tayari amekwishabainisha umbile la mtu basi damu inayomtoka inazingatiwa kuwa ni damu ya uzazi. Hivyo hatoswali. Wanachuoni wamesema kwamba umbile la mtu kutoka kwenye kipomoko hicho linaweza kubainika pale kinapotimiza siku 81. Kipindi hichi ni chini ya miezi mitatu. Kama una uhakika kwamba mimba iliporomoka ndani ya miezi mitatu, basi damu aliyopata ni damu ya kawaida ambayo hatakiwi kuacha swalah kwa ajili yake.
Ni lazima kwa dada huyu muulizaji ajikumbushe mwenyewe. Ikiwa kipomoko kimetoka kabla ya siku 81, basi anatakiwa kulipa swalah zake. Akiwa hajui ni swalah ngapi ameacha basi atatakiwa kujitahidi na alipe kwa mujibu wa vile inavyomtilia nguvu dhana yake kwamba hakuswali.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: 60 su-aal wa jawaab fiy Ahkaam-il-Haydhw, uk. 26
- Imechapishwa: 27/07/2021
Swali 29: Mimi ni mwanamke ambaye mimba yangu imeporomoka ndani ya mwezi wa tatu mwaka mmoja uliopita na sikuswali mpaka niliposafika. Nimeambiwa kwamba nilipaswa kuswali. Nifanye nini na mimi sijui idadi halisi ya siku?
Jibu: Kinachofahamika kwa wanachuoni ni kwamba mwanamke akiporomosha mimba ya miezi mitatu haswali. Kwa sababu mwanamke akiporomosha kipomoko ambaye tayari amekwishabainisha umbile la mtu basi damu inayomtoka inazingatiwa kuwa ni damu ya uzazi. Hivyo hatoswali. Wanachuoni wamesema kwamba umbile la mtu kutoka kwenye kipomoko hicho linaweza kubainika pale kinapotimiza siku 81. Kipindi hichi ni chini ya miezi mitatu. Kama una uhakika kwamba mimba iliporomoka ndani ya miezi mitatu, basi damu aliyopata ni damu ya kawaida ambayo hatakiwi kuacha swalah kwa ajili yake.
Ni lazima kwa dada huyu muulizaji ajikumbushe mwenyewe. Ikiwa kipomoko kimetoka kabla ya siku 81, basi anatakiwa kulipa swalah zake. Akiwa hajui ni swalah ngapi ameacha basi atatakiwa kujitahidi na alipe kwa mujibu wa vile inavyomtilia nguvu dhana yake kwamba hakuswali.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: 60 su-aal wa jawaab fiy Ahkaam-il-Haydhw, uk. 26
Imechapishwa: 27/07/2021
https://firqatunnajia.com/41-ibaadah-ya-mwanamke-ambaye-mimba-imeporomoka-ndani-ya-miezi-mitatu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)