37. Zakaah wanapaswa kupewa watawala

Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:

“Inafaa na ni sahihi kuwapa zakaah sawa wakiwa wema au waovu.”

MAELEZO

Miongoni mwa haki za watawala ni kuwapa zakaah. Zakaah wanatakiwa kupewa wao au manaibu wao na si wengineo. Yule mwenye kutoa zakaah kumpa mwengine asiyekuwa wao basi ni lazima kwake kuilipa tena.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Itmaam-ul-Minnah, uk. 140
  • Imechapishwa: 30/04/2019