153- ´Abdullaah bin ´Amr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kwamba kuna mtu alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Uislamu upi bora. Akajibu:
“Kulisha chakula na kumsalimia unayemjua na usiyemjua.”
154- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hamtoingia Peponi mpaka muamini na hamtoamini mpaka mpendane. Nisikuelezeni kitu ambacho mkikifanya kitawafanya kupendana? Enezeni Salaam baina yenu.”
155- ´Ammaar bin Yaasir (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:
“Kuna sifa tatu. Mwenye kuwa nazo basi amekusanya imani; uadilifu juu ya nafsi yako, kuwatolea Salaam viumbe na kujitolea katika kipindi kizito.”
156- ´Imraan bin Husayn (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:
“Kuna mtu alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ
“as-Salaam ´alaykum.”
Akamuitikia kisha mtu yule akakaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Kumi.” Kisha akaja mtu mwengine na kusema:
السَّلام عَلَيْكُمْ وَرحمة الله
“as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah.”
Akamuitikia kisha mtu yule akakaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ishirini.” Kisha akaja mtu mwengine na kusema:
السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللهِ وَبَرَكَاته
“as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaahi wa Barakaatuh.”
Akamuitikia kisha mtu yule akakaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Thalathini.”
157- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watu walio na haki zaidi kwa Allaah ni wale wenye kuanza kwa Salaam.”
158- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Inatosheleza katika kundi linalopita mmoja wao akatoa Salaam na inatosheleza katika kundi linalokaa mmoja wao akaitikia Salaam.”
159- Anas (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipita pembezoni mwa watoto wanaocheza akawatolea Salaam.”
160- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wakati mmoja wenu anapofika katika majlisi awatolee Salaam. Akitaka kukaa, akae. Akitaka kusimama na kwenda awatolee Salaam. [Salaam] ya kwanza haina haki zaidi kuliko ile ya pili.”
- Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 100-102
- Imechapishwa: 21/03/2017
153- ´Abdullaah bin ´Amr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kwamba kuna mtu alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Uislamu upi bora. Akajibu:
“Kulisha chakula na kumsalimia unayemjua na usiyemjua.”
154- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hamtoingia Peponi mpaka muamini na hamtoamini mpaka mpendane. Nisikuelezeni kitu ambacho mkikifanya kitawafanya kupendana? Enezeni Salaam baina yenu.”
155- ´Ammaar bin Yaasir (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:
“Kuna sifa tatu. Mwenye kuwa nazo basi amekusanya imani; uadilifu juu ya nafsi yako, kuwatolea Salaam viumbe na kujitolea katika kipindi kizito.”
156- ´Imraan bin Husayn (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:
“Kuna mtu alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ
“as-Salaam ´alaykum.”
Akamuitikia kisha mtu yule akakaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Kumi.” Kisha akaja mtu mwengine na kusema:
السَّلام عَلَيْكُمْ وَرحمة الله
“as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah.”
Akamuitikia kisha mtu yule akakaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ishirini.” Kisha akaja mtu mwengine na kusema:
السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللهِ وَبَرَكَاته
“as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaahi wa Barakaatuh.”
Akamuitikia kisha mtu yule akakaa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Thalathini.”
157- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watu walio na haki zaidi kwa Allaah ni wale wenye kuanza kwa Salaam.”
158- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Inatosheleza katika kundi linalopita mmoja wao akatoa Salaam na inatosheleza katika kundi linalokaa mmoja wao akaitikia Salaam.”
159- Anas (Radhiya Allaahu ´anhu) amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipita pembezoni mwa watoto wanaocheza akawatolea Salaam.”
160- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wakati mmoja wenu anapofika katika majlisi awatolee Salaam. Akitaka kukaa, akae. Akitaka kusimama na kwenda awatolee Salaam. [Salaam] ya kwanza haina haki zaidi kuliko ile ya pili.”
Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 100-102
Imechapishwa: 21/03/2017
https://firqatunnajia.com/37-kutoa-salaam/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)