Mapambano yakawa mapambano kwelikweli na nusura ikateremshwa. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akajitahidi na akaomba du´aa kwelikweli mpaka nguo yake ya juu ikawa inamshuka kutoka mabegani mwake. Abu Bakr (Radhiya Allaahu ´anh) akawa anaipandisha na kusema:
“Ee Mtume wa Allaah! Usijichoshe kumuomba Mola wako sana kiasi hivo. Hakika atakutimizia ahadi Aliyokupa.”
Na huku Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
“Ee Allaah! Kikiangamia kikundi hichi basi hutoabudiwa ardhini.”
Hapo ndipo Allaah (Ta´ala) akateremsha:
إِذْ تَسْتَغِيثُونَ رَبَّكُمْ فَاسْتَجَابَ لَكُمْ أَنِّي مُمِدُّكُم بِأَلْفٍ مِّنَ الْمَلَائِكَةِ مُرْدِفِينَ
“Wakati mlipomuomba uokovu Mola wenu Naye akakuitikieni kwamba: “Hakika Mimi nitakusaidieni kwa Malaika elfu wafuatanao mfululizo.”[1]
Kisha akasinzia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Baada ya muda kidogo akainua kichwa chake na kusema:
“Pata bishara njema ee Abu Bakr! Huyu hapa Jibriyl akiwa na udongo kwenye meno yake ya mbele.”[2]
[1] 08:09
[2] al-Bayhaqiy katika ”Dalaa-il-un-Nubuwwah” (3/81).
- Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Kathiyr ad-Dimashqiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Fusuwl fiy Siyrat-ir-Rasuwl, uk. 50-51
- Imechapishwa: 09/10/2018
Mapambano yakawa mapambano kwelikweli na nusura ikateremshwa. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akajitahidi na akaomba du´aa kwelikweli mpaka nguo yake ya juu ikawa inamshuka kutoka mabegani mwake. Abu Bakr (Radhiya Allaahu ´anh) akawa anaipandisha na kusema:
“Ee Mtume wa Allaah! Usijichoshe kumuomba Mola wako sana kiasi hivo. Hakika atakutimizia ahadi Aliyokupa.”
Na huku Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:
“Ee Allaah! Kikiangamia kikundi hichi basi hutoabudiwa ardhini.”
Hapo ndipo Allaah (Ta´ala) akateremsha:
إِذْ تَسْتَغِيثُونَ رَبَّكُمْ فَاسْتَجَابَ لَكُمْ أَنِّي مُمِدُّكُم بِأَلْفٍ مِّنَ الْمَلَائِكَةِ مُرْدِفِينَ
“Wakati mlipomuomba uokovu Mola wenu Naye akakuitikieni kwamba: “Hakika Mimi nitakusaidieni kwa Malaika elfu wafuatanao mfululizo.”[1]
Kisha akasinzia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Baada ya muda kidogo akainua kichwa chake na kusema:
“Pata bishara njema ee Abu Bakr! Huyu hapa Jibriyl akiwa na udongo kwenye meno yake ya mbele.”[2]
[1] 08:09
[2] al-Bayhaqiy katika ”Dalaa-il-un-Nubuwwah” (3/81).
Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Kathiyr ad-Dimashqiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Fusuwl fiy Siyrat-ir-Rasuwl, uk. 50-51
Imechapishwa: 09/10/2018
https://firqatunnajia.com/34-duaa-ya-mtume-kabla-ya-vita-vya-badr-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)