34. Dalili ya thelathini na mbili kutoka katika Sunnah kwamba Allaah yuko juu ya viumbe

32- Abu Zur´ah Twaahir bin Muhammad bin Twaahir al-Maqdisiy alisomewa na mimi huku nasikiza: Abu Mansuur Muhammad bin al-Husayn amekukhabarisheni: Abu Twalhah al-Qaasim bin Abiyl-Mundhir ametuhadithia: Abul-Hasan ´Aliy bin Ibraahiym bin Salamah ametuhadithia: Abu ´Abdillaah Muhammad bin Yaziyd bin Maajah ametuhadithia: Muhammad bin ´Abdil-Malik bin Abiysh-Shawaarib ametuhadithia: Abu ´Aaswim al-´Abbaadaaniy ametuhadithia: al-Fadhwl ar-Raqqaashiy ametuhadithia, kutoka kwa Muhammad bin al-Munkadir, kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah aliyesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Wakati watu wa Peponi watapokuwa wakineemeka kwa neema zao watazungukwa na na nuru. Pindi wataponyanyua vichwa vyao kuielekea watamuona Mola wao (´Azza wa Jall) akiwa juu yao. Atasema: “Enyi watu wa Peponi! Amani iwe juu yenu!” Halafu akasoma:

سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ

“Mola Mwingi wa huruma atawasalimia akisema: “Amani!”[1]

Atawatazama na wao watamtazama. Hawatokielekea kitu kingine katika neema za Peponi midhali wanamtazama Yeye. Hatimaye Atajificha nao na ibaki nuru Yake na baraka Zake juu yao katika majumba yao.”[2]

[1] 36:58

[2] Ibn Maajah (184), al-Bazzaar (2253) na Abu Nu´aym katika ”Hilyat-ul-Awliyaa’” (6/208). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katka ”Dhwa´iyf Sunan Ibn Maajah”, uk. 17.

  • Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ithbaatu Swifat-il-´Uluww, uk. 122-124
  • Imechapishwa: 12/06/2018