31. Ni ipi hukumu ya kufunga bila ya kuswali?

Swali 31: Ni ipi hukumu ya kufunga bila ya kuswali?

Jibu: Hivi kweli inawezekana kufunga bila ya kuswali? Kufanya nguzo ya nne na kuacha nguzo ya pili? Mtu awe muislamu kunahitajia kukubali uwajibu wa swawm na wa hajj tofauti na swalah. Haitoshi kukubali uwajibu wake tu. Asiyeswali ni wajibu kumtaka atubie. Ima atubie au auawe hali ya kuwa ni kafiri. Haya ndio maoni sahihi ilihali wanachuoni wengi wanasema kuwa auawe hali ya kuwa ni mtenda dhambi.

Wale wasiomkufuruisha asiyeswali wanasema atauawa hali ya kuwa ni mtenda dhambi. Dalili zinafahamisha kuwa asiyeswali ni kafiri ambaye damu na mali yake ni halali. Ikisihi kama kweli anaacha swalah kwa kukusudia, ni mwenye kuritadi. Katika hali hiyo anatakiwa kuwekwa mbele ya hakimu wa Kishari´ah na amtake kutubia. Ima atubie au amhukumu kifo kikafiri.

Tukisema kuwa ni kafiri basi hatutotakiwa kumtembelea pindi atapokuwa mgonjwa wala kumswalia pindi atapokufa. Mali yake itakuwa ni fai ya waislamu. Asiwarithi warithi wake na wala wao wasimrithi. Aidha mke wake anatengana na yeye moja kwa moja. Hukumu zote hizi anatakiwa kutekelezewa.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaas-Swiyaam, uk. 45-46
  • Imechapishwa: 12/06/2017