Swali 31: Ni ipi hukumu ya ambaye ananyanyua mikono yake wakati ambapo Khatwiyb anawaombea waislamu katika Khutbah ya pili pamoja na kunitajia dalili[1]?
Jibu: Kunyanyua mikono ni kitu hakikuwekwa katika Shari´ah katika Khutbah ya ijumaa wala katika Khutbah ya ´iyd. Ni mamoja kwa imamu wala maamuma. Kilichowekwa katika Shari´ah ni kumnyamazia Khatwiyb na kuitikia “Aamiyn” du´aa yake. Mtu afanye hivo kati yake yeye na nafsi yake pasi na kunyanyua sauti. Kuhusu kunyanyua mikono ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akinyanyua mikono yake katika Khutbah ya ijumaa wala katika Khutbah za ´iyd. Pindi baadhi ya Maswahabah walipowaona baadhi ya viongozi wananyanyua mikono yao katika Khutbah ya ijumaa waliwakemea kitendo hicho na wakawaambia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akiinyanyua.
Akiomba du´aa ya kuteremshiwa mvua katika Khutbah ya ijumaa hapo atanyanyua mikono yake katika ile hali ya kuomba kuteremshiwa mvua. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akinyanyua mikono yake katika hali hii. Akiomba kuteremshiwa mvua katika Khutbah ya ijumaa au katika Khutbah ya ´iyd basi imesuniwa kwake kunyanyua mikono yake kwa ajili ya kumwigiliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/338-339).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 70-71
- Imechapishwa: 02/12/2021
Swali 31: Ni ipi hukumu ya ambaye ananyanyua mikono yake wakati ambapo Khatwiyb anawaombea waislamu katika Khutbah ya pili pamoja na kunitajia dalili[1]?
Jibu: Kunyanyua mikono ni kitu hakikuwekwa katika Shari´ah katika Khutbah ya ijumaa wala katika Khutbah ya ´iyd. Ni mamoja kwa imamu wala maamuma. Kilichowekwa katika Shari´ah ni kumnyamazia Khatwiyb na kuitikia “Aamiyn” du´aa yake. Mtu afanye hivo kati yake yeye na nafsi yake pasi na kunyanyua sauti. Kuhusu kunyanyua mikono ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akinyanyua mikono yake katika Khutbah ya ijumaa wala katika Khutbah za ´iyd. Pindi baadhi ya Maswahabah walipowaona baadhi ya viongozi wananyanyua mikono yao katika Khutbah ya ijumaa waliwakemea kitendo hicho na wakawaambia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akiinyanyua.
Akiomba du´aa ya kuteremshiwa mvua katika Khutbah ya ijumaa hapo atanyanyua mikono yake katika ile hali ya kuomba kuteremshiwa mvua. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akinyanyua mikono yake katika hali hii. Akiomba kuteremshiwa mvua katika Khutbah ya ijumaa au katika Khutbah ya ´iyd basi imesuniwa kwake kunyanyua mikono yake kwa ajili ya kumwigiliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/338-339).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 70-71
Imechapishwa: 02/12/2021
https://firqatunnajia.com/31-hakunyanyuliwi-mikono-katika-khutbah-ya-ijumaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)