133- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Yule anayetaka kusafiri aseme kuwaambia wale anaotaka kuwaacha:
أَسْتَوْدِعُكُمْ الله الذِي لا تَضيعُ وَدَائِعُهُ
”Ninawaacha chini ya ulinzi wa Allaah ulinzi ambao hauendi hivi hivi.”
134- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kile kinachoachwa chini ya ulinzi wa Allaah basi Allaah Hukihifadhi.”
135- Saalim amesema:
“Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) alikuwa akisema kumwambia mtu ambaye anataka kusafiri: “Njoo karibu yangu. Nitaagana na wewe kama jinsi Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyokuwa akiagana na sisi:
أَسْتَودعُ اللهَ دِينَكَ وأمانَتَكَ وَخَواتِيمَ أَعْمَالِكَ
”Ninaacha Dini yako, amana yako na kitendo chako cha mwisho katika ulinzi wa Allaah.”
136- Kuna mtu alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
“Ee Mtume wa Allaah! Ninataka kusafiri. Niwazadie kitu.” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Allaah Akuzawadie Taqwa.” Akasema: “Nipe zaidi.” Akasema: “Akusamehe dhambi zako.” Akasema: “Nipe zaidi.” Akasema: “Akusahilishie kheri popote ulipo.”
137- Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kwamba kuna mtu alisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Mimi nataka kusafiri. Niusie.” Akasema: “Mche Allaah na sema “Allaahu Akbar” katika kila sehemu ya kupanda.” Wakati mtu yule alipotoka pale akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
اللَّهُمَّ اطْوِ لَهُ الْبُعْدَ وَهَوِّنْ عَلَيْهِ السَّفرَ
“Ee Allaah! Mfupishie umbali wake na msahilishie safari yake.”
- Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 91-93
- Imechapishwa: 21/03/2017
133- Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Yule anayetaka kusafiri aseme kuwaambia wale anaotaka kuwaacha:
أَسْتَوْدِعُكُمْ الله الذِي لا تَضيعُ وَدَائِعُهُ
”Ninawaacha chini ya ulinzi wa Allaah ulinzi ambao hauendi hivi hivi.”
134- Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kile kinachoachwa chini ya ulinzi wa Allaah basi Allaah Hukihifadhi.”
135- Saalim amesema:
“Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) alikuwa akisema kumwambia mtu ambaye anataka kusafiri: “Njoo karibu yangu. Nitaagana na wewe kama jinsi Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyokuwa akiagana na sisi:
أَسْتَودعُ اللهَ دِينَكَ وأمانَتَكَ وَخَواتِيمَ أَعْمَالِكَ
”Ninaacha Dini yako, amana yako na kitendo chako cha mwisho katika ulinzi wa Allaah.”
136- Kuna mtu alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
“Ee Mtume wa Allaah! Ninataka kusafiri. Niwazadie kitu.” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Allaah Akuzawadie Taqwa.” Akasema: “Nipe zaidi.” Akasema: “Akusamehe dhambi zako.” Akasema: “Nipe zaidi.” Akasema: “Akusahilishie kheri popote ulipo.”
137- Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kwamba kuna mtu alisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Mimi nataka kusafiri. Niusie.” Akasema: “Mche Allaah na sema “Allaahu Akbar” katika kila sehemu ya kupanda.” Wakati mtu yule alipotoka pale akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
اللَّهُمَّ اطْوِ لَهُ الْبُعْدَ وَهَوِّنْ عَلَيْهِ السَّفرَ
“Ee Allaah! Mfupishie umbali wake na msahilishie safari yake.”
Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 91-93
Imechapishwa: 21/03/2017
https://firqatunnajia.com/31-duaa-wakati-wa-safari/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)