177- Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kamwe hakukuwa mkate wa shayiri kwa familia ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]
178- Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anaweza kushinda nyusiku nyingi za kufuatana akiwa na njaa na familia yake haina chakula cha jioni. Mara nyingi walikuwa wakila mkate wa shayiri.”[2]
179- Kulisemwa kuambiwa Sahl bin Sa´d (Radhiya Allaahu ´anh):
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikula mkate mweupe?” Akasema: “Sikumuona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akila mkate mweupe mpaka alipokutana na Allaah (´Azza wa Jall).”[3]
180- ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Familia ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hawakula wakashiba mkate wa ngano nyusiku tatu za kufuatana tangu alipofika al-Madiynah mpaka alipofariki.”[4]
181- ´Urwah bin az-Zubayr amesema:
“Shangazi yangu alinambia: “Ee mwangu! Ninaapa kwa Allaah tulikuwa tunaweza kumaliza nyusiku arubaini na nyumbani kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakukongwi moto na wala hakuashwi taa.” Nikamuuliza: “Mlikuwa mnaishi kwa kitu gani?” Akasema: “Viwili vyeusi; tende na maji na hakuna kingine.”[5]
182- ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Kitanda cha Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kilikuwa kimetengenezwa kwa ngozi iliyoshinikizwa makuti.”[6]
[1] at-Tirmidhiy (2464) ambaye amesema: ”Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
[2] at-Tirmidhiy (2465), Ibn Maajah (3347) na Ahmad (1/255). at-Tirmidhiy amesema: ”Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
[3] at-Tirmidhiy (2469) na Ibn Maajah (3335). at-Tirmidhiy amesema: ”Hadiyth ni Swahiyh.”
[4] al-Bukhaariy (8/121) na Muslim (18/105).
[5] al-Bukhaariy (8/121) na Muslim (18/107).
[6] al-Bukhaariy (8/121) na Muslim (14/58).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 112-115
- Imechapishwa: 18/03/2017
177- Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kamwe hakukuwa mkate wa shayiri kwa familia ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]
178- Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anaweza kushinda nyusiku nyingi za kufuatana akiwa na njaa na familia yake haina chakula cha jioni. Mara nyingi walikuwa wakila mkate wa shayiri.”[2]
179- Kulisemwa kuambiwa Sahl bin Sa´d (Radhiya Allaahu ´anh):
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikula mkate mweupe?” Akasema: “Sikumuona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akila mkate mweupe mpaka alipokutana na Allaah (´Azza wa Jall).”[3]
180- ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Familia ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hawakula wakashiba mkate wa ngano nyusiku tatu za kufuatana tangu alipofika al-Madiynah mpaka alipofariki.”[4]
181- ´Urwah bin az-Zubayr amesema:
“Shangazi yangu alinambia: “Ee mwangu! Ninaapa kwa Allaah tulikuwa tunaweza kumaliza nyusiku arubaini na nyumbani kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakukongwi moto na wala hakuashwi taa.” Nikamuuliza: “Mlikuwa mnaishi kwa kitu gani?” Akasema: “Viwili vyeusi; tende na maji na hakuna kingine.”[5]
182- ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Kitanda cha Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kilikuwa kimetengenezwa kwa ngozi iliyoshinikizwa makuti.”[6]
[1] at-Tirmidhiy (2464) ambaye amesema: ”Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
[2] at-Tirmidhiy (2465), Ibn Maajah (3347) na Ahmad (1/255). at-Tirmidhiy amesema: ”Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
[3] at-Tirmidhiy (2469) na Ibn Maajah (3335). at-Tirmidhiy amesema: ”Hadiyth ni Swahiyh.”
[4] al-Bukhaariy (8/121) na Muslim (18/105).
[5] al-Bukhaariy (8/121) na Muslim (18/107).
[6] al-Bukhaariy (8/121) na Muslim (14/58).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 112-115
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/30-maisha-khafifu-aliokuwa-nayo-mtume/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)