3. Uzuri wa mwanamke uko usoni

Ya pili: Allaah Amesema:

وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ

“… hivyo waangushe khimari zao mpaka vifuani mwao.”

Khimari ni vazi ambalo mwanamke anafunika kichwa chake. Ikiwa ameamrishwa kufunika kifua basi vilevile ameamrishwa kufunika uso. Hilo linafanywa ima ni kwa sababu ni jambo ambalo lisiloweza kuepukwa au kwa sababu ya kipimo [Qiyaas]. Ikiwa ni wajibu kufunika kifua na matiti basi ni jambo la wajibu zaidi kufunika uso ambapo ni sehemu ya uzuri na fitina. Wale ambao wanachotaka ni uzuri wanacholenga huwa ni uso. Uso ukiwa mzuri hawatilii umuhimu mkubwa kitu kingine. Pindi inaposemwa kuwa mwanamke fulani ni mzuri mtu anacholenga huwa ni uso wake. Ni jambo lenye kuonyesha ya kwamba uso ndio mahala uzuri ulipo kwa njia zote. Vipi basi mtu atafikiria kuwa Shari´ah hii yenye hekima imeamrisha kufunika kifua na kuacha uso ukaonekana?

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Hijaab, uk. 7-8
  • Imechapishwa: 26/03/2017