29. Ni wajibu kukata swawm pale tu jua linapozama?

Swali 29: Ni wajibu kwa mfungaji kukata swawm pale tu jua linapozama[1]?

Jibu: Sio wajibu. Imependekezwa kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema pindi alipokataza kuunganisha swawm:

“Anayetaka kuendelea na swawm basi aendelee mpaka wakati wa daku.”[2]

[1] Kutoka “Fath-ur-Rabb al-Waduud” (1/250).

[2] ad-Daarimiy (1705).

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaas-Swiyaam, uk. 44
  • Imechapishwa: 12/06/2017