Download

116-

اللهم اهدني فيمن هديت, وعافني فيمن عافيت, وتولني فيمن توليت, وبارك لي فيما أعطيت, وقني شر ما قضيت, فإنك تقضي ولا يقضى عليك, وإنه لا يذلّ من واليتَ, [ولا يعزّ من عاديت], تباركت ربنا وتعاليت

“Ee Allaah! Niongoze pamoja na wale Uliowaongoza, uniafu pamoja na wale Uliowaafu, Uniangalie pamoja na wale Unaowaangalia, Unibariki katika kile Ulichotoa na Unilinde kutokamana na shari kwa yale Uliyohukumu. Kwani hakika Wewe ndiye mwenye kuhukumu na wala huhukumiwi. Hakika hatwezeki yule Uliyemfanya mpenzi na wala hapati nguvu yule Uliyemfanya adui. Umebarikika, Mola Wetu, Umetukuka.”[1]

117-

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِرِضـاكَ مِنْ سَخَطِـك، وَبِمُعـافاتِـكَ مِنْ عُقوبَـتِك، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْـك، لا أُحْصـي ثَنـاءً عَلَـيْك، أَنْـتَ كَمـا أَثْنَـيْتَ عَلـى نَفْسـِك

“Ee Allaah! Hakika mimi najilinda kwa radhi Zako kutokamana na hasira Zako, kwa msamaha Wako kutokamana na adhabu Yako na najilinda Kwako kutokamana Nawe – mimi siwezi kuzidhibiti sifa Zako; hakika Wewe ni kama ulivyojisifu Mwenyewe.”[2]

118-

اللّهُـمَّ إِيّـاكَ نعْـبُدْ، وَلَـكَ نُصَلّـي وَنَسْـجُد، وَإِلَـيْكَ نَسْـعى وَنَحْـفِد، نَـرْجو رَحْمَـتَك، وَنَخْشـى عَـذابَك، إِنَّ عَـذابَكَ بالكـافرين ملْحَـق. اللّهُـمَّ إِنّا نَسْتَعـينُكَ وَنَسْتَـغْفِرُك، وَنُثْـنـي عَلَـيْك الخَـيْرَ، وَلا نَكْـفُرُك، وَنُـؤْمِنُ بِك، وَنَخْـضَعُ لَكَ وَنَخْـلَعُ مَنْ يَكْـفرُك

”Ee Allaah! Wewe pekee ndiye tunakuabudu, Kwako tunaswali na tunasujudu, Kwako tunakimbilia na tunakutumikia, tunataraji rehma Zako na tunaogopa adhabu Yako; kwani hakika adhabu Yako ni yenye kuwafikia makafiri. Ee Allaah! Hakika sisi tunakutaka msaada, tunakuomba msamaha, tunakusifu kwa kheri na wala hatukukufuru, tunakuamini Wewe, tunakunyenyekea na tunamuepuka anayekukufuru.”[3]

[1] Watunzi wa “as-Sunan” wanne, Ahmad, ad-Daarimiy, al-Haakim na al-Bayhaqiy na pia ilioko ndani ya mabano ni ya al-Bayhaqiy. Tazama ”Swahiyh-ut-Tirmidhiy” (01/144), ”Swahiyh Ibn Maajah (01/194)” na ”Irwaa´-ul-Ghaliyl” (02/172) vya al-Albaaniy.

[2] Watunzi wa “as-Sunan” wanne na Ahmad. Tazama ”Swahiyh-ut-Tirmidhiy” (03/180), ”Swahiyh Ibn Maajah (01/194)” na ”Irwaa´-ul-Ghaliyl” (02/175).

[3] al-Bayhaqiy katika ”as-Sunan al-Kubraa” na ameisahihisha cheni ya wapokezi wake (02/211). Shaykh al-Albaaniy katika ”Irwaa´-ul-Ghaliyl”: “Cheni ya wapokezi hii ni Swahiyh” (02/170). Ni yenye kuishilia kwa ´Umar.

  • Mhusika: Shaykh Sa´iyd bin ´Aliy bin Wahf al-Qahtwaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Huswn-ul-Muslim
  • Imechapishwa: 28/04/2020