28. Muadhini aadhini kwanza kisha ndio akate swawm?

Swali 28: Sisi tuna muadhini ambaye watu wanamfuata katika adhaana ya Maghrib. Anaadhini pale tu jua linapozama. Je, akate swawm kwanza kisha ndio aadhini? Au anatakiwa aadhini kwanza kisha ndio akate swawm kwa kuzingatia kuwa watu wanamfuata yeye[1]?

Jibu: Yote mawili yanajuzu. Akiwa na uhakika kuwa jua limeshazama akate swawm kwa tende na anywe maji halafu aadhini. Anaweza vilevile akaadhini kwanza kisha ndio akate swawm. Napendekeza hili la pili.

[1] Kutoka “Fath-ur-Rabb al-Waduud” (1/252).

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaas-Swiyaam, uk. 43-44
  • Imechapishwa: 12/06/2017