28. Aina ya tano ya majina ya haramu

5- Majina ya kigeni kama ya kituruki, ya kifursi na ya kishenzi yasiyopata nafasi katika kiarabu. Mfano wa majina hayo ni Nariymaan, Sherihaan, Shaadiy (likiwa na maana ya ngedere kwenye lugha yao) na Jiyhaan.

Kuhusu majina yanayoisha kwa herufi “t” kama Hikmat, ´Iswmat, Najdat, Hibat, Mirfat na Ra-fat, asli ni ya kiarabu. Lakini kwa vile yanaisha kwa “t” badala ya “h” sio ya kiarabu tena.

Hali kadhalika majina ya kuisha kwa herufi “iy” kama Ramziy, Husniy, Rushdiy, Haqqiy, Majdiy na Rajaaiy. Asli ya majina haya ni ya kiarabu. Midhali yanaisha kwa “iy” sio ya kiarabu tena kwa sababu iy hii ni jambo la kifursi na kituruki.

Kuhusu jina Faqiy Misri, ni ufupisho wa “Faqiyh”.

Mfano wa majina ya kifursi ni yale yenye kuisha kwa “uuyah” kama Siybuuyah. Kuna ambao wamefikisha mpaka majina tisini na mbili yenye kuisha kwa “uuyah”.

Katika kiurdu wanaweka herufi “iy” ikiwa jina ni la kike. Rahmaan inakuwa Rahiyman naa Kariym inakuwa Kariyman.

  • Mhusika: ´Allaamah Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tasmiyat-ul-Mawluwd, uk. 24-25
  • Imechapishwa: 18/03/2017