La tano: Mwanamke damu yake ikikauka ndani ya ada, inafaa kufanya jimaa na mume wake. Ni jambo ambalo halikuchukizwa kabisa. Hata hivyo ni jambo lenye kuchukiza kufanya naye jimaa akikauka katika damu ya uzazi wake ndani ya siku arubaini. Hii ndio kauli yenye kujulikana katika madhehebu [ya Hanaabilah].

Kauli sahihi ni kuwa haikuchukizwa kabisa kufanya naye jimaa. Hii ndio kauli ya wanachuoni wengi. Machukizo ni hukumu ya Kishari´ah inayohitajia dalili ya Kishari´ah. Hakuna katika masuala haya dalili isipokuwa ile aliyotaja Imaam Ahmad kutoka kwa ´Uthmaan bin Abiyl-´Aasw na kwamba mke wake alimjia ndani ya zile siku arubaini ambapo akasema:

“Usinikaribie.”

Hili halilazimishi kuwa imechukizwa. Huenda alisema hivo kwa njia ya usalama kwa kukhofia kwamba hakuwa na yakini juu ya kutwahatika kwake, damu yake kurudi kwa sababu ya jimaa au sababu nyengineyo na Allaah ndiye anajua zaidi.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Dimaa’ at-Twabiy´iyyah lin-Nisaa’ http://www.ibnothaimeen.com/all/books/article
  • Imechapishwa: 30/10/2016